Askari wa Jeshi la wananchi wa Tanzania waliotayarishwa
maalum kwa ajili ya kubeba mashada ya mau kwa ajili ya kuweka katika Kaburi la
Marehemu Mzee Abeid Amani Karume Mwanamapinduzi wa Zanzibar na Rais wa Kwanza
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa ASP.
Rais
wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, Makamu
wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Makamu
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif, Balozi Ali Karume na Balozi
Mdogo wa China Zanzibar Balozi Tai Yanlia na kulia Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni
Jenerali S.A.Ndomba.na Muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Ahmeid
Ameir, akiwa amekaa katika kiti.wakisubiri kuweka Mashada ya Mau katika kaburi
la Marehemu Mzee Abeid Amani Karume baada ya kusomwa kwa Dua ya kumuombea
iliofanyika katika jingo la Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akiwa na Mama Fatma Karume wakiwa na Wake wa Viongozi katika hafla ya kuweka Mashada ya Mau katika kaburi la marehemu Mzee Abeid Amani Karume wakati wa kumuombea Dua iliofanyika katika Jengo la Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.kulia Mke wa Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Zakia Bilal na Mke wa Rais Mstaafu wa Zanzibar Mama Shadya Karume
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akiwa na Mama Fatma Karume wakiwa na Wake wa Viongozi katika hafla ya kuweka Mashada ya Mau katika kaburi la marehemu Mzee Abeid Amani Karume wakati wa kumuombea Dua iliofanyika katika Jengo la Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.kulia Mke wa Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Zakia Bilal na Mke wa Rais Mstaafu wa Zanzibar Mama Shadya Karume
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiweka
Shada la mau katika kaburi la Marehemu Mzee Abeid Amani Karume, baada ya dua ya
kumuombea iliofanyika katika Jengo la Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar na
kuhudhuriwa na Wananchi mbalimbali katika hitma hiyo.
Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Shada la mau katika kaburi la
Marehemu Mzee Abeid Amani Karume, baada ya dua ya kumuombea iliofanyika katika
Jengo la Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar na kuhudhuriwa na Wananchi
mbalimbali katika hitma hiyo.
MNADHIMU Mkuu wa JWTZ Luteni
Jenerali S.A.Ndomba akiweka Shada la mau katika kaburi la
Marehemu Mzee Abeid Amani Karume, baada ya dua ya kumuombea iliofanyika katika
Jengo la Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.
Balozi
Mdogo wa China Zanzibar Balozi Tai
Yanlia, akiweka Shada la mau katika kaburi la Marehemu Mzee Abeid Amani Karume,
baada ya dua ya kumuombea iliofanyika katika Jengo la Afisi Kuu ya CCM
Kisiwandui Zanzibar.akiwakilisha Mabalozi Wadogo walioko Zanzibar.
Muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar Mhe Ahmeid Ameir , akiweka Shada la mau katika
kaburi la Marehemu Mzee Abeid Amani Karume, baada ya dua ya kumuombea
iliofanyika katika Jengo la Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.ni mmoja wa
Wanamapinduzi ya Zanzibar aliyeshiriki na Marehemu Mzee Karume kuikombo
Zanzibar
Mtoto wa Marehemu Mzee Abeid Amani Karume Balozi Ali
Karume akiweka Shada la Mau kwa niaba ya Familiya katika kaburi la Baba yao
wakati wa kumuombea Dua iliofanyika katika Jengo la Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui
Zanzibar ikiwa ni kumbukumbu ya kumkumbuka Jamadari wa Mapinduzi ya Zanzibar
Mzee Karume.
Mufti
Mkuu wa Zanzibar Shekh Saleh Omar Kabi akisoma dua katika kaburi la Marehemu
Mzee Abeid Amani Karume, ikiwa ni dua maalum ya kumkumbuka Mzee Karume
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mama Mwanamwema Shein, akiwa na Mama
Fatma Karume,Bi Yasmin Aloo na kushoto Mke wa Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania Mama Zakia Bilal, Mke wa Rais Mstaaf wa Zanzibar Mama
Shadya Karume na Bi Asha Abdallah wakiitikia dua wakiwa katika kaburi la Mzee
Karume.
Viongozi wa Serekali wakiwa katika eneo la kaburi la Mzee
Karume wakiitikia dua iliokuwa ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar.
Baba Askofu Mkuu wa Zanzibar wa Kanisa la Anglikana Mkunazini Zanzibar Askofo , Michael
Hafidh, akimuombe Marehemu Mzee Abeid
Amani Karume wakati wa kumbukumbu ya marehemu kumuombea dua, iliofanyika katika
jingo la Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.
Kiongozi wa Madhehebu ya Hindu Zanzibar Bangwanji
Mshaba akisoma dua katika kaburi la marehemu Mzee Abeid Amani Karume wakati wa
dua ya kumuombea iliofanyika Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.
Viongozi
wa Serekali wakiwa katika viwanja vya Afisi Kuu ya CCM kuhudhuria Dua ya
kumuombea Marehemu Mzee Abeid Amani Karume, kutoka kulia Mhe Haroun Ali
Suleiman, Mhe Bernard Membe na Mhe Mark Mwandosa wakifuatila hafla hiyo ya dua.
Baadhi
ya Wananchi waliohudhuria katika Hitma ya kumuombea Marehemu Mzee Abeid Amani
Karume iliofanyika leo katika jingo la Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif
Hamad akimsikiliza Rais Mstaaf wa Zanzibar Dk. Amani Karume wakiwa katika
viwanja vya Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar, baada ya kumalizika kwa hafla
ya Dua.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi,
akizungumza na Shekh Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Shekh. Alhad Mussa na Mhe
Bernard Membe wakiwa katika viwanja vya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar baada ya
kumalizika kwa hafla ya dua leo asubuhi.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif
Hamad, akiagana na Meya wa Mji wa Zanzibar Mhe Khatib Abdurahaman Khatib, baada
ya kumalizika kwa hafla ya kumuiombea Dua Marehemu Mzee Abeid Amani Karume
Jamadari wa Mapinduzi ya Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi,
akizungumza na Shekh Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Shekh. Alhad Mussa na Mhe
Bernard Membe wakiwa katika viwanja vya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar baada ya
kumalizika kwa hafla ya dua leo asubuhi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi,
akiagana na Meya wa Mji wa Zanzibar Mhe Khatib Abdurahaman Khatib na Wananchi
waliohudhuria hafla ya kumuiombea Dua Marehemu Mzee Abeid Amani Karume Jamadari
wa Mapinduzi ya Zanzibar.
Spika
wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Pandu Ameir Kificho akifurahia jambo na
Mhe Mark Mwandosa wakiwa katika viwanja vya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar
walipohudhuria hafla ya kisomo cha kumuombea dua Marehemu Mzee Abeid Amani
Karume.
Waziri
wa Biashara, Viwanda na Masoiko Mhe Nassor Mazrui, akizungumza na waandishi wa
habari maendeleo yalioletwa na Mzee Karume wakati wa uhai wake
Baba
Askofo Micheil Hafidh akizungumza na Waandishi wa habari wa vyombo
mbalimbali baada ya kumalikiza kwa hafla
ya dua.
Balozi Ali Karume akizungumza na Waandishi wa habari baada
ya kumalizika kwa hafla ya dua
Muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar Mhe Ahmeid Ameir
akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika hafla ya dua ya
kumuombea Mzee Karume iliofanyika katika Afisi Kuu ya CCM Zanzibar .
Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa Mhe
Bernard Membe akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vilioko
Zanzibar wakati alipohudhuria hitma ya kumuombea Marehemu Mzee Abeid Amani
Karume iliofanyika katika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.
SubhaanaAllah siku hizi hatuna mashekhe tenakwani wao wanashindwa kukemea ouvu wa aina yoyote kwa kutaka kuwaridhisha watawala.Serikali haina dini kama wasemavyo lakoni watu wa dini na dini yetu ni Al Islam sasa kitabu gani kinacho ruhusu kufanya kumbukumbu na baya zaidi kuweka mauwa.Kuombea dua kwa maiti wetu ni sawa kabisa kwani wanihitaji huko waliko lakini haya mauwa ............Kama nimekosea naomba mwenye elimu anisaidie
ReplyDeletemwenyezi mungu amlipe kwa yale aliyoyatanguliza kwa mikono yake ameen , kila mtu atabeba zigo lake mwenyewe , visomo hivyo havifiki popote ndugu watawala na nyie vile vile mkirudi kwa mungu mtalipwa kwa yale mnayoyatanguliza hata tukisoma hitma kila siku ni bure tu , kila mtu hulipwa kwa amali zake hii kujidanganya na hitma na mashekhe wetu feki hao
ReplyDelete