Habari za Punde

Amani, utulivu na mshikamano ndio misingi pekee ya kuleta maendeleo endelevu Zanzibar.


  
STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Zanzibar                                                                           7.7.2015
---
WANANACHI wa Mkoa wa Kaskazini Unguja wameeleza kuwa amani, utulivu na mshikamano ndio misingi pekee ya kuleta maendeleo endelevu hapa Zanzibar.

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Meja Mstaafu Juma Kassim Tindwa aliyasema hayo, wakati akitoa shukurani kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein huko katika viwanja vya Ikulu ndogo Mkokotoni.

Aidha, Mama Mwanamwema Shein naye aliungana na akina mama wenzake wa Mkoa huo katika futari hiyo ya pamoja iliyoandaliwa na Alhaj Dk. Shein kwa ajili ya wananchi wa Mkoa huo.

Katika maelezo yake Mhe. Tindwa alisisitiza azma ya Dk. Shein ya kuendeleza amani, utulivu na mshikamano miongoni mwa Wazanzibari na kumpongeza juhudi anazozichukua kwa niaba ya wananchi wa Mkoa huo.

Mhe. Tindwa alieleza kuwa amani ndio tunu ya taifa, hivyo kuna kila sababu ya kuilinda, kuidumisha na kuitetea kwa hali zote huku akisisitiza kwa yeyote atakaejaribu kuvunja amani aripotiwe kwenye vyombo vinavyohusika.

Alisisitiza kuwa Waislamu wote ni ndugu hivyo kuna kila sababu ya wananchi wa Zanzibar kuendelea kuishi kwa amani, maelewano na mapenzi makubwa miongoni mwao ili kumpwekeshwa MwenyeziMungu.

Nae Maalim Khamis Hassan kutoka Mkoa huo, akitoa neno la shukurani kwa niaba ya wafutarishwa alisisitiza haja ya kuendeleza ushirikiano baina ya wananchi wote.

Maalim Khamis alitumia fursa hiyo kutoa neno la shukurani kwa niaba ya wazee wa mkoa huo kwa futari hiyo huku wakimuombea dua Alhaj Dk. Shein azidi kuendelea kuiongoza Zanzibar kwa amani, utulivu, mshikamano na maelewano makubwa.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.