Habari za Punde

Zantel yatoa msaada wa vyakula kwa makundi maalum ya wazee Zanzibar


 NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii , Vijana , Wanawake na Watoto, Nd. Msham Juma Khamis akimkabidhi msaada , Pili Ahmada wakati wa makabidhiano ya msaada wa vyakula uliotolewa na Kampuni ya simu ya Zantel.

Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel, bw Mohammed Mussa akizungumza machache kabla ya makabidhiano ya msaada wa vyakula uliotolewea na Zantel kwa ajili ya Wazee

 Naibu Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazee Zanzibar (JUWAZA), Mwadini Kutenga akiwakaribisha wageni wakati wa shughuli ya makabidhino ya msaada wa chakula kutoka kwa Zantel kwenda kwa jumuiya ya wazee Zanzibar
Sehemu ya wazee waliokabidhiwa msaada wa vyakula na Zantel.

Zanzibar, 15 July 2012: Kampuni ya simu za mikononi ya Zantel leo imetoa msaada wa vyakula kwa ajili ya mwezi wa Ramadhani kwa makundi maalumu ya wazee hapa visiwani Zanzibar.

Msaada huo unajumuisha sukari, unga wa ngano pamoja na mchele umetolewa katika hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika leo.

Kampuni ya Zantel upande wa Zanzibar imeainisha wazee zaidi ya 120 wenye uhitaji wa vyakula kwenye mwezi huu wa Ramadhani walio chini ya jumuiya ya wazee hapa Zanzibar.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo kwa wazee, Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel-Zanzibar, bwana Mohammed Mussa, amesema ni kawaida kwa kampuni ya Zantel kusaidia makundi mbalimbali ya kijamii katika kipindi hiki cha Ramadhani.

'Tuna furaha sana leo kuweza kusaidia jamii hii ya wazee ambao mara nyingi wamekuwa wanasahaulika, kwani tunaamini wazee ni sehemu muhimu sana ya jamii ndio maana Zantel leo tumeamua kutoa msaada huu ambao unatutofautisha sana na makampuni mengine katika vipaumbele vyetu' alisema Mussa.


Mussa aliongeza kuwa kama kampuni ya simu inayoongoza Zanzibar, Zantel mara zote imekuwa mfano katika shughuli zake za kijamii na vipaumbele vyake kiujumla.

Akizungumza wakati wa shughuli hiyo, mgeni rasmi ndugu Msham Abdallah, ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ustawi wa Jamii Zanzibar, alisema anaipongeza Zantel kwa kushirikiana na serikali kuyasaidia makundi ya wazee.

‘Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali katika kulisaidia kundi hili la wazee, kwahiyo ni furaha kwetu leo kuona Zantel imekuwa ya kwanza kusaidia kundi hili leo’ alisema bwana Abdallah.

Akitoa neno la shukrani kwa kampuni ya Zantel, naibu mwenyekiti wa jumuiya ya wazee Zanzibar, Bwana Mwadini Kutenga, alisema anawashukuru Zantel kwa msaada huo, akisema umekuja kwa wakati mufaka hasa ukizingatia kuwa wanakaribia kuadhimisha sikukuu ya Idi.

1 comment:

  1. Hii kampuni bado inatumia jina la Zantel ? Kwani si imeshauzwa hii kwa kampuni ya Tigo ? Naona hata siyafaham haya makampuni ......mwenye uledi nayo anijulishe

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.