Bwana
Yussuf Shoka Hamad akimkabidhi kioo cha
Kompyuta Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Mtemani, Wingwi Bi Wahida Saleh Hamad.
‘Nia yangu ni kuleta mapinduzi ya kweli kwa jamii katika sekta ya elimu. Mapinduzi ya kweli kwa ulimwengu wa sasa yanatokana na kutegemea sana maendeleo ya sayansi na teknolojia. Hivyo, katika kipindi hiki cha miaka mitano (2015/20) nimenuilia kuanzisha maktaba za kisasa (digital libraries) kwa shule zote za Wingwi ili kusukuma mbele maendeleo ya elimu!’
Aidha mhisani huyo alisema kwamba wakati umefika kwa wanakijiji wa Wingwi kuamka na kuipa kipaumbele sekta ya Elimu kwa watoto wao kwani Elimu ndio silaha tosha inayoweza kuleta Mapinduzi nchini. Pia aliwasisitiza wanakamati wa shule hiyo, kuthamini michango inayotolewa na wahisani na wazazi wa wanafunzi kwa kutunza na kuenzi kila msaada unaopatiwa shuleni hapo.
Akitoa mchango wake mbele ya kamati katika hafla hiyo, Mwalimu mkuu wa shule ya Mtemani Bi Wahida Saleh alisema, anashukuru sana kupokea vifaa hivyo na ameahidi kuvitunza na kuvitumia ipasavyo ili kuweza kuleta matunda yanayotazamiwa kupatikana kutokana na uanzishwaji wa maktaba hiyo shuleni hapo.
Naye, mdau wa Elimu na mwanakamati wa shule hiyo Bwana Shoka Hamad Abeid ameinasihi kamati na jamii kwa ujumla kuvitunza vifaa hivyo na kuvienzi kwani kufanya hivyo kutepelekea lengo zima la kulete ufanisi shuleni hapo kufikiwa;
‘Kwa hakika changamoto kubwa linalotukabili kwa sasa sio kupata misaada bali ni jinsi gani tunavitunza na kuiendeleza misaada hiyo. Kwa sisi wanakamati, walimu na wanafunzi, tunao wajibu mkubwa wa kuvitunza vifaa hivi. Kinyume na hivyo tutaishia kupokea na kuomba misaada tu kila siku bila kufikia malengo tunayoyatarajia.’ Alisema Bwana Shoka.
Wakati huo huo, mdau na mtaalamu wa mambo ya takwimu wa kamati hiyo , Bwana Suleiman Said alimuomba Bwana Yussuf Shoka kuwapatia laptops zitakazoweza kusaidia walimu kuandaa masomo yao kwa ufanisi zaidi hata wawapo majumbani.
Na: Moh’d Said
Shule ya msingi ya mtemani Wingwi
iliyoko Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, imekabidhiwa vifaa vya
kisasa kwa ajili ya ujenzi na uanzishaji wa maktaba ya kisasa (Digital Library)
inayaotarajiwa kufunguliwa hivi karibuni.
Tukio
hilo lilifanyika leo katika viwanja vya shule ya mtemani mbele ya kamati ya
shule hiyo ambapo muhisani na mdau wa
maendeleo nchini ambaye pia ni mhadhiri kutoka chuo kikuu cha London, SOAS,
Bwana Yussuf Shoka Hamad alikabidhi zawadi hizo kama sehemu ya ahadi zake
alizozitoa mwaka jana katika hafla ya kuwazawadia wanafunzi waliofaulu vizuri
darasa la saba mwaka 2013/14.
Akikabidhi
zawadi hizo, Bwana Yussuf Shoka Hamad alisema;
‘Nia yangu ni kuleta mapinduzi ya kweli kwa jamii katika sekta ya elimu. Mapinduzi ya kweli kwa ulimwengu wa sasa yanatokana na kutegemea sana maendeleo ya sayansi na teknolojia. Hivyo, katika kipindi hiki cha miaka mitano (2015/20) nimenuilia kuanzisha maktaba za kisasa (digital libraries) kwa shule zote za Wingwi ili kusukuma mbele maendeleo ya elimu!’
Aidha mhisani huyo alisema kwamba wakati umefika kwa wanakijiji wa Wingwi kuamka na kuipa kipaumbele sekta ya Elimu kwa watoto wao kwani Elimu ndio silaha tosha inayoweza kuleta Mapinduzi nchini. Pia aliwasisitiza wanakamati wa shule hiyo, kuthamini michango inayotolewa na wahisani na wazazi wa wanafunzi kwa kutunza na kuenzi kila msaada unaopatiwa shuleni hapo.
Akitoa mchango wake mbele ya kamati katika hafla hiyo, Mwalimu mkuu wa shule ya Mtemani Bi Wahida Saleh alisema, anashukuru sana kupokea vifaa hivyo na ameahidi kuvitunza na kuvitumia ipasavyo ili kuweza kuleta matunda yanayotazamiwa kupatikana kutokana na uanzishwaji wa maktaba hiyo shuleni hapo.
Naye, mdau wa Elimu na mwanakamati wa shule hiyo Bwana Shoka Hamad Abeid ameinasihi kamati na jamii kwa ujumla kuvitunza vifaa hivyo na kuvienzi kwani kufanya hivyo kutepelekea lengo zima la kulete ufanisi shuleni hapo kufikiwa;
‘Kwa hakika changamoto kubwa linalotukabili kwa sasa sio kupata misaada bali ni jinsi gani tunavitunza na kuiendeleza misaada hiyo. Kwa sisi wanakamati, walimu na wanafunzi, tunao wajibu mkubwa wa kuvitunza vifaa hivi. Kinyume na hivyo tutaishia kupokea na kuomba misaada tu kila siku bila kufikia malengo tunayoyatarajia.’ Alisema Bwana Shoka.
Wakati huo huo, mdau na mtaalamu wa mambo ya takwimu wa kamati hiyo , Bwana Suleiman Said alimuomba Bwana Yussuf Shoka kuwapatia laptops zitakazoweza kusaidia walimu kuandaa masomo yao kwa ufanisi zaidi hata wawapo majumbani.
Shule
ya msingi mtemani ni miongoni mwa vituo vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
inayotegemea zaidi nguvu za jamii na wahisani wazalendo katika kujipatia
maendeleo shuleni hapo ambapo kwa sasa imeshapiga hatua mbali mbali za
kimaendeleo ikiwamo ya ujenzi wa maktaba ya kisasa na maabara ya kompyuta
ambayo inatarjiwa kufunguliwa katika siku za usoni.
No comments:
Post a Comment