Bi Mauwa Khamis Saateni wa shehia
ya Vitongoji wilaya ya Chakechake Pemba, akiwa ni mmoja kati ya wanawake 93 wa
ukanda wa Mashariki wa kisiwa cha Pemba, ambao baada ya kupata elimu ya
ushawishi na utetezi wa haki za wanawake na wanawake kumiliki ardhi na kushinda
kesi hiyo mahakama ya ardhi, akiwa kwenye shamba lake ambalo kwa muda wa miaka zaidi
ya 20, lilikuwa likishikiliwa na mama yake wa kambu na sasa limerudi mikononi
mwake baada ya mafunzo ya VECA (picha na
Haji Nassor, PEMBA)
Ni baada ya mafunzo ya kutambua
haki zao yalitolewa na VECA
Na Haji Nassor, PEMBA
‘’HIVI nnavyozugumza nawe, tayari
ardhi yangu nimeshaikomboa kutoka mikononi mwa familia yangu, na sasa
nshaipanda mahindi’’,alidakiza Bibi Mauwa Khamis Saateni wa Vitongoji
Chakechake Pemba,
Nilimtaka
arejee maneno hayo, akarejea kama yalivyo hapo juu, na akasema alikaa zaidi ya
miaka 20 akiwa hana habari na ardhi yake, ilio kuwa mikononi mwa mama yake wa
kambo.
Lakini
baada ya Jumuia ya uhifadhi wa mazingira ya Vitongoji wilaya ya Chakechake
Pemba, ‘VECA’ kumpa mafunzo ya ushawishi na utetezi wa haki za wanawake na
wanawake kumiliki ardhi, hayo ndio matokeo.
“Sasa
nna eneo langu karibu ekeri nne, lakini papatu ilipita, maana nilikwenda
mahakama ya ardhi kwa muda wa minne, lakini bwana jaji mwisho akasema ardhi nirejeshewe
mweyewe’’,alifafanua.
Mwanamke
huyu jemedari alikuwa na hadithi refu juu ya mafunzo alioyapata hadi kuweza
kutia mikononi ardhi yake, ambapo awali aliona kama mzaha mafunzo hayo.
‘’Kwe
kweli VECA walipotuita kutupa mafunzo hayo, mimi niliona kama semina za kawaida
tukachukue posho turudi nymbani, lakini yale mafunzo waliotupa yalikua darsa
tosha kwangu’’,aliweka wazi.
Mauwa
(48), baada ya kuwiva kimasomo kwamba na wao wanahaki ya kumiliki ardhi, na
wana haki ya kwenda mahakamani, ndipo alipoanza safari ya kudai ardhi yake.
“Ardhi
yake ya ekari nne ilikua inamilikiwa na mama yangu wa kambo, kwa miaka zaidi ya
20, maana tokea mwaka 1994 alikuwa akiitumia bila ya mimi
kufahamu’’,alikumbuka.
Baada
ya kumaliza mafunzo, alianza kumuuliza mama yake juu ya ardhi yake, ingawa
hakupata jawabu nzuri jambo ambalo, baadae aliitisha kikao cha pamoja na kulizungumza
hilo na hawakumfahamu.
Binti
Saateni, aliamua kwenda mahakama ya ardhi, na baadae wakakutana juu ya kiriri
na mama yake wa kambo, ambapo baada ya nenda rudi ya mahakamani, miezi minne
baadae, alikabidhiwa ardhi yake.
‘’Mimi
hadi leo sijaamini kwamba ardhi yangu nimeipata, maana mama hakua na hoja, na
bwana jaji (hakimu) akaamua kuwa nikabidhiwe, na yeye bila ya kinyongo
alinipa’’,alisema kwa furaha.
Hawakukosea
wahenga waliposema, mwisho wa maji ni tope………..na ndio maana sasa bibi Mauwa,
anadunda kwa kupanda mihindi kwenye ardhi yake akiwa na hati zote husika.
‘’Siku
niliokabidhiwa na mahakama ardhi yangu, ndio nilipoona umuhimu wa yale mafunzo
tuliopewa na VECA, na nasema ahasante jumuia hii’’,alisema kwa shauku.
Bibi
Mauwa Khamis Saateni kwa sasa, baada ya kufanikiwa kuikomboa ardhi yake ambayo
kwa muda wa zaidi ya miaka 20, ilikuwa mikononi kwa familia yake, mwanzoni mwa
mwaka 2014, tayari kwa sasa ametinga tena mahakamani.
Safari
hii akiwa kwenye kizimba cha mahakama ya ardhi, anaidai nyumba yake ya urithi,
ambayo kwa sasa haimo mikononi mwake.
‘’Tena
nailaumu sana ‘VECA’ mafunzo waliotupa sisi wanawake wa ukanda wa mashiriki wa
kisiwa cha Pemba, kama wengetupa miaka kumi (10) iliopita, wanawake sisi
twengekuwa mbali’’,alieleza kwa furaha.
Kesi
hiyo ya kudai nyumba inatarajiwa kunguruma tena kwenye mahakama ya ardhi mwezi
ujao mwaka huu wa 2015, mweyewe akiwa na tamaa kubwa ya kufanyiwa haki na Idara
ya mahakama ya ardhi.
Bi
Mauwa sio pekee ambaye alifanikiwa kupata ardhi yake baada ya mafunzo hayo,
lakini hakimu wa mahakama hiyo Salim Hassan Bakari alisema mafunzo hayo
yaliamsha idadi kubwa kesi za ardhi.
‘’Baada
ya VECA kumaliza mradi wao kwa mwaka wa kwanza, wa ushawishi na utetezi wa haki
za wanawake na wanawake kumilikia ardhi, kesi za wanawake pekee zilifikia 93,
kwenye mahakama yangu’’,aliweka wazi Hakimu.
Aliddadavua
kuwa, kati ya kesi hizo zinazohusu ardhi pekee za wanawake wa ukanda wa
mashariki wa kisiwa cha Pemba, kesi 43 zimeshafanyiwa kazi na kutolewa maamuzi.
Miongoni
mwa kesi hizo 17, wanawake walishinda akiwemo Bibi Mauwa Khamis Saateni, na
sasa ardhi zao wameshakabidhiwa wenyewe na Mahakama na hati zote wameshapewa.
Ingawa
kesi nyengine 26, wanawake walishindwa, kutokana na kukosa vithibitisho halisi,
ingawa kimatiki inaonekana wamedhulumiwa na wanaume (kaka, ndugu, baba) zao.
Hakimu
Salim Hassan Bakari, alitamka kuwa kesi 50 bado hazijamalizika na zinaendelea
katika mahakama ya ardhi, zikiwahusu wanawawake wa ukanda wa mashirikia wa
kisiwa cha Pemba.
‘’Unajua
hata makarani wangu walishituka, baada ya kuona wanapokea kesi mfululizo za
wanawake ndani ya miezi minne, tena na kushinda maana walipata ujasiri wa
kusimama mahakamani’’, alisema.
VECA ambayo ilipata ufadhili kutoka kwa ‘the
foundation for civil society’ wa shilingi 135,000,000 kwa ajili ya mradi wa
ushawishi na utetezi wa haki za wanaweake na wanawake kumilikia ardhi, kwa
hakika umezaa matunda,
Maneno
hayo ualiiungwa mkono na kijana Khamis Haji Makame, ambae nae alibahatika
kushiriki mafunzo hayo yalioandaliwa na VECA kwa kushirikiana na ‘foundation’.
“Mimi
nilikua sijui kuwa pia wanawake wanahaki ya kumiliki ardhi, nilijua ni mwanamme
tu, maana ndie kiongozi wa familia na mwanamke yeye daima awe nyuma’’, alisema.
Khamis
alisema mafunzo hayo ya ‘VECA’ ndio yaliomuamsha na kumpa uwelewa mpana, kwamba
kumbe mwanamke kumiliki ardhi sio fursa bali ni haki yake.
Baada
ya mafunzo hayo, Khamis yeye ameshamsaidia dadayake (Fatma) kumuelekeza kwamba,
amdai kaka yao haki yake ya ardhi, walioirithi na kujimilikisha yeye kwa zaidi
ya miaka 10 sasa.
‘’Dada
Fatma baada ushawishi na utetezi wangu, na kufanya kikao cha familia, sasa dada
ana ardhi yake na kaka aliitoa rahisi, bila ya kwenda mahakama ya ardhi’’,alisema
Khamis.
Kubwa
Khamis analolitaka kutoka kwa ‘VECA’ ni kuhakikisha mafunzo kama hayo, yanakua
endelevu maana wapo wanawake kadhaa wengine hayajawafikia mafunzo hayo.
Mratibu
wa mradi huo Mohamed Najim Omar, yeye alisema kwamba jamii ya kijiji cha Vitongiji
na ya ukanda wa mashariki kwa ujumla, itajengwa na VECA kwa kushirikiana na ‘the
foundation for civil society’ ambayo imekuwa ikiwanunga mkono kila mara.
Mradi
huo, ambao ni mwa miaka mitano, ulianza tokea mwaka 2012, na ukitarajiwa
kufunga nanga yake mwaka 2015, ingawa alisema yapo matunda kabla ya mradi
kumalizika.
Mafanikio
makubwa wanayojivunia ni kuona kuwa walengwa wa mradi huo ambao ni wanawake na
jamii kwa jumla, wameanza kupata miguu ya kusimama na kudai haki zao.
‘’Wanawake wetu wa ukanda wa mashariki,
walikua na dhana potofu kwamba, kwa vile mwanamme ndie msisimamizi wa familia,
basi umiliki wa ardhi ni wajibu wake’’,alisema.
Kwa
sasa hilo Mratibu anajivunia, na kusema idadi ya wanawake 93 kutoka ukanda wa
mashariki wa kisiwa cha Pemba, kupeleka mashauri yao mahakama ya ardhi sio
dogo.
Muhasibu
wa mradi huo, bibi Sifuni Ali Haji, yeye alisema alipata mshangao wakati wa
utoaji wa mafunzo hayo, jinsi wanawake wa ukanda wa mshiriki walivyokuwa
wakitoa ushuhuda.
‘’Mwanamke
anasimama kwenye mafunzo anasema yeye ardhi yake anayo kaka yake au mjomba wake
na hujui kinachoendelea, lakini leo si haba ‘foundation’ lazima tujivunie
VECA’’,alibainisha.
Sifuni
alisema walinza na utekelezaji wa mradi huo kwa, mikutano ya hadhara,
ikifuatiwa na mafunzo ya kamati za maendeleoa za vijiji 36 vya ukanda wa
mashariki ikiwa ni pamoja na Uwandani, Ole, Kangagani, Furaha, Vitongoji na
Pujini.
Watu
120 kwa hatua ya awali walitajwa kufaidika na mafunzo hayo, ambapo baadae VECA,
ilikutana na viongozi wa dini na masheha wa shehia zilizo ukanda wa mashariki,
huku nayo makundi maalumu yakihusishwa.
Mafunzo
hayo yalikuwa na lengo lilelile na kuwapa uwelewa makundi hayo, kwamba yanaweza
kufanya ushawishi na utetezi wa haki za wanawake na wanawake kumiliki ardhi.
Ndio
maana sheha wa shehia ya Vitongoji Salim Ayoub, yeye aliesma kama jamii
itayafanyiakazi mafunzo hayo, migogoro ya kuwania ardhi hasa kwa wanawake
yataondoka.
Sheikh
Omar Ali Mohamed, yeye alisema ni kosa kidini mwanamme kujimilikisha ardhi ya
urithi, zawadi au ya kununua, ambayo ni ya mwamke na kutumia vibaya nguvu na
madaraka yake.
Afisa
tawala wilaya ya Chakechake Rashid Hadid Rashid, alinukuliwa akisema, juhudi za
taasisi ys ‘Foundation’ wa kuifadhili VECA wala fedha zao hazipotei, maana wapo
wanawake ambao leo wanajivunia kupata aradhi zao.
Mohamed
Kombo Hamad, alisema kutokana na uwelewa walionao wanawake hao, kwa sasa
wamekuwa wakijitokeza wenyewe wakati anapotokezea mwekezaji na kutaka kununua
aradhi.
‘’Zamani
ilikua ardhi ya mwanamke inauzwa na mwanamme, au kaka yake na kisha
kilichopatikana hakipati, lakini sasa ni tofauti.
Wengi
wanadhani kwamba endapo VECA itahitimisha mradi wake huo mwaka 2015, basi
wanawake na jamii ya ukanda wa mashariki, suala la ufahamu wa sheria na sera za
ardhi litakuwa pana na kupunguza migogoro ya ardhi.
No comments:
Post a Comment