Habari za Punde

Moto wateketeza ekari 20 Pemba

VIONGOZI wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa kaskazini Pemba, wakiongozwa na mkuu wa Mkoa huo Mhe:Omar Khamis Othman, wakikagua ekari 20 za msitu wa wanajamii zilizoteketea kwa moto zenye thamani ya Milioni 200/=, huko Kikunguni Kigongoni Shumba Viamboni Wilaya ya Micheweni Kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 LICHA ya wananchi na kikosi cha Zimamoto na Uwokozi Wilaya ya Wete Kisiwani Pemba, kujitahidi kuuzima moto ulioteketeza zaidi ya Ekari 20 za msitu wa hifadhi ya jamii zenye thamani ya shulingi Milioni 200/=, huko Kikunguni kigongoni shumba Viambani lakini bado baadhi ya maeneo moto huo haukukubali kuzimika.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)


 SHEHA wa Shehia ya Mihogini Shumba Viamboni Wilaya ya Micheweni Salim Said Salim, akizungumza na waandishi wa habari mbali mbali, juu ya athari iliyopatikana baada ya zaidi ya Ekari 20 kuteketea kwa moto za msitu wa Hifadhi ya wanajamii wa Kikunguni Kigongoni shumba Viamboni Wilaya ya Micheweni kisiwani pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 KATIMU mkuu wa Wilaya ya Micheweni, ambaye pia ni mkuu wa Wilaya ya Wete Mhe:Hassan Khatib Hassan, akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua eneo la msitu lililoathirika na moto na kuteketeza zaidi ya Ekari 20 zenye thamani ya shilingi Milioni 200/=, huko Kikunguni Kigongoni Shumba Viamboni Wilaya ya Micheweni Kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

 MKUU wa Mkoa wa kaskazini Pemba Mhe: Omar Khamis Othman, akitoa tamko la Serikali ya Mkoa wake na kuwapa pole wananchi waliopata hasara ya kuunguliwa msitu wao wa wanajamii na kuteketeza zaidi ya ekari 20 zenye thamani ya Milioni 200, huko Kikunguni Kigongoni Shumba Viamboni Wilaya ya Micheweni Kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 KAMANDA wa Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba Mhe: Hassan Nassir Ali, akizungumza na waandishi wa habari juu ya tamko la Jeshi la polisi, dhidi ya watu waliofanya hujma za kuichoma moto msitu wa wanajamii na kutekeketeza zaidi ya Ekari 20 zenye thamani ya shilingi Milioni 200, huko kikunguni Kigongoni Shumba Viamboni Wilaya ya Micheweni Kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.