Habari za Punde

Wananchi wakiri midahalo ‘PACSO’ yawaamsha kulinda amani na utuliv

 BAADHI ya waandishi wa habari walioshiriki uzinduzi wa mradi wa jukwaa la amani, wakati na baada ya uchaguzi mkuu, unaoendeshwa na mwenvuli wa asasi ya kiraia Pemba ‘PACSO’ uzinduzi huo umefanyika skuli ya maandalizi Madungu mjini Chaka chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).  
 MRATIBU wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, Fatma Khamis Hemed, akiwasilisha mada ya umuhimu wa amani wakati na baada ya uchaguzi mkuu, kwenye mdahalo ulioandaliwa na asasi ya kirais ‘PACSO’ kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa asasi hiyo, Ali Said Hamad na kushoto ni Mwenyekiti wake Omar Ali Omar, mdahalo huo umefanyika skuli ya sekondari ya Fidel Castro, (Picha na Haji Nassor, Pemba)
MWANACHAMA wa Jumuia ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar ‘JUWAUZA’ Hidaya Mjaka Ali, akichangia mada kwenye mdahalo wa jukwaa la amani wakati na baada ya uchaguzi mkuu, mdahalo huo, umeandaliwa na asasi ya kiraia ‘PACSO’ Pemba, na kufanyika skuli ya sekondari ya Fidel Castro, (Picha na Haji Nassor, Pemba). 


Wasema ‘Foundation’ hawakukosea kuiwezesha asasi hiyo

Na Haji Nassor, Pemba

“HE…. kumbe huu ndio umuhimu wa amani kabla, wakati na baada ya uchaguzi’’,wameonyesha uwelewa wananchi wa mkoa wa kusini Pemba.

Wamejisifia kuwa, wanasiasa wamekuwa wakiwachanganya juu ya amani, maana wapo wengine wamekuwa wakitoa maneno ya vijembe wakati wakinadi sera zao.

Wapiga kura hawa kutoka wilaya za Chake chake na Mkoani, wamejigamba kuwa sasa, wameshapata uwelewa mkubwa kupitia midahalo ya PACSO.

Wakati wakimuhadisia mwandishi wa makala haya, kutaka kujua ni nani aliwaita kwenye midahalo hiyo, walisema kuwa ni Mmwevuli wa Mtandao wa Asasi za kiraia Kisiwani Pemba, ‘PACSO.

Wakizungumza nami wananchi hawa wanasema ‘PACSO’ midahalo hiyo imewaweka wazi kwani hapo awali walikuwa wakibabaishwa na wanasiasa.

Uwelewa walioupata, kupitia midahalo hiyo, imeweza kuwasaidia sana maana kwa sasa wanachofanya ni kuhakikisha wanakatazana vile viashirio vyote vya uvujifu wa amani.


Akizungumza kwenye mdahalo uliofanyika  Skuli ya sekondari ya Fidel csatro wilaya ya Chake chake Omar Khamis Ameir wa Chake chake anasema suala la maelekezo ya wanasiasa kulinda kura halikuwa na tija.

“Kumbe hata kulinda kura, kwa maana ya kukaa mita 200, ni jambo ambalo linaweza kuzaa matunda mabaya, lakini haya nimeyafahamu kwenye mdahalo wa ‘PACSO’ alisema.

Asha Haji Makame, nae anasema kuwa kabla ya kushiriki katika mdahalo huo, hakuwa na uwelewa mpana wa jinsi nafasi yake ya kulinda amani na utulivu.

“Mimi kupitia mdahalo huo, ndio nimepata uelewa kumbe kila mwananchi anayonafasi ya kufanikisha uchaguzi mkuu kuwa wa amani na utulivu, maana moja ni kuwaelimisha wengine’’,alieleza.

Nae Juma Kombo Hassan wa Jimbo la Wawi wilaya ya Chake chake alielezea kupata taaluma kubwa juu ya kutunza amani na umuhimu wake.

Mwanajuma Haji Mmaka, wa Mkoani anasema midahalo kama hiyo ingefaa sana kufanyika hata kabla ya kuanza kwa kampeni.

“Mimi naona midahalo kama hii ya jukwaa la amani wakati na baada ya uchaguzi, ingefanyia kabla ya kuanza kwa kampeni ili sisi wananchi tupate elimu pana’’,alifafanua.

Katika midahalo hiyo, Mkurugenzi Mtendaji  wa ‘PACSO’ Ali Said Hamad, yeye anasema kila mmoja anayo nafasi ya kuufanikisha uchaguzi mkuu kuwa wa amani na utulivu.


Mkurugenzi huyo, anasema mwandishi wa habari, wanasiasa, wapiga kura, wanawake, watu wenye ulemavu na vijana wanaweza kutuliza mizuka yao na  amani iliopo ikadumu.

“Mimi naamini kwa hizi wilaya mbili tulizozifikia na wananchi kushiriki vyema,  basi fedha za ‘Foundation for Civill Society’ hazikutumika bure, maana hata wananchi walihamasika juu ya umuhimu wa kutunza amani’’, alibainisha Mkurugenzi huyo wa PACSO.

Kwa ujumla wananchi zaidi ya 500 ndani ya mkoa wa kusini Pemba ambao inaumndwa na majimbo tisa, walifikiwa na taaluma hiyo kupitia midahalo ya wazi na kuibua changamoto kadhaa na kupelekea uchaguzi kuwa wa amani.

Kwa mujibu wa andiko la mradi, walengwa walikuwa ni 230, ingawa kutokana na wananchi kuhamasika na kuona kuwa kwenye asasi hiyo ndiko watapata taaluma, walivuuka lengi na kufikia 500.

“Wananchi wengine wamekuja hata wakualikwa, waliposikia tu kuwa mdahalo wa amani walikuja, tulipowaliuza walisema kwenye vyama vyao hubaniwa taaluma hiyo”, alisema Makamu Mwneyekiti wa PACSO Aisha Abdalla Rashid.

Hakusita kusema inaonyesha wananchi walikuwa na hamu na midahalo ya asasi ya kirai, na hasa kutokana na kutoegemea upande mmoja wa chama wala serikali.

Hata hivyo ameiomba ‘Foundation for Civil Society’ ya Da –es Salaam kuendelea kuwawezesha kila muda ili Tanzania iwe na wananchi wanaofahamu wajibu na haki zao katika kulinda amani na utulivu.

Mwenyekiti wa PACSO, Omar Ali Omar anasema miongoni mwa makundi yaliofaidika na midahalo hiyo ni viongozi wa dini, wanawake, wenye ulemavu, vijana pamoja na wanasiasa.

“Unuaju kila mmoja anafahamu athari na faida za amani, lakini kwa makusudi ‘PACSO’ imeamua kuusaka mradi huu ili kukumbushana’’,alifafanua.

Akiwasilisha mada kwenye mdahalo uliofanyika skuli ya sekondari ya Fidel castro, Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, Fatma Khamis Hemed, alisema suala la amani ni tunu ya taifa.

Anasema kama hivyo ndivyo, ni vyema kila mwananchi kuona ananafasi ya kutunza amani na utulivu uliopo, ili taifa libakie kwenye hali hii hata baada ya uchaguzi.

“Jamani amani haichezewi, amani haijaribiwi kuvunjwa na wala haina mbadala wake, sasa lazima tuitunzeni sana ‘’,alisisitiza.

Mwanaharakati wa kijamii Abubakar Mohamed Ali, akiwasilisha mada ya umuhimu wa amani, kwenye ukumbi wa ZAYEDESA Mkoani Pemba, alisema wanaotaka kuvunja amani waangali nchi jirani.

Yeye anasema PACSO, imepata mradi huo wakati mwafaka maana, kila mmojana anadhani suala la kuhimizana amani na utuli kama vile ni kazi ya vyombo vya ulinzi na usalama pakee.

“Lazima suala la kutunza amani na utulivu, tusilipe kipaumbele tu hata baada ya uchaguzi kumalizika, lakini hata baadae maana Tanzania ipo’’,alisema.

Yeye aliipongeza sana PACSO, kutokana na kuona umuhimu wa kuwa na mradi huo ambao, ndio uliotoa dira na mwanga kwa jamii, maana wanasiasa wamekuwa wakiwachanganya wapiga kura wao.

Ingawa Makamu Mwenyekiti wa PACSO, Aisha Abdalla Rashid, yeye anasema kama kweli jamii ikiyaapuza maelekezo yasio na tija ya wanasiasa, basi amani ya kudumu itapatikana.

“Wapo wanasiasa wameku wakitoa lugha za viashirio vya uvunjifu wa amani, na wapo wananchi wamekuwa wakiunga mkono, sasa hilo sio jambo jema’’,alifafanua.

Baadhi ya wananchi waliipongeza PACSO kutokana na uamuzi wake wa kuingilia kati, suala la kutoa elimu ya umuhimu wa amani, na hasa kwa vile vyama vimekuwa vikitoa elimu ambayo ndani yake inawakalakini.  

Kwenye mafanikio, basi huwa na changamoto hazikai mbali, maana PACSO nayo ilikumbana nazo, ikiwa ni pamoja na mradi huo kuja wakati tayari kampeni zimeshawiva.

Jengine ni kukosekana hasa kwa wale wagombea husika kwa maana ya wabunge na wawakilishi, maana wengi wao walishajipangia ratiba za mikutano ya kampeni.

Ilionekana ilikuwa vigumu kwa kundi moja wapo la walengwa hao, kuhudhuria wao wenyewe kwenye midahalo ya PACSO, kutokana na kutingwa na safari ya kusaka kura.

“Kila kitu fedha, na fedha ikiwa kidogo huwezi kufanya kitu, nasi fedha shilingi 15 milioni zilikuwa hazitoshi, kama the foundation wengietupa alau shilingi 45 milioni basi twengefanya kila kitu’’,alifafanua Sifuni Ali Haji.

Yeye ameiomba foundation wakati mwengine kuwapatia fedha zenye kiwango kikubwa na kupewa walau mwezi mmoja kabla ya kampeni, ili kuhakikisha wanafikia walengwa wote.

Mmwevuli wa Mtandao wa Asasi za kiraia Kisiwani Pemba (PACSO), ambao umeanzishwa mwaka 2006 na unao wanachama 76 asasi za kiraia na umeshawahi kupatiwa ufadhili miradi mitano na Foundation ikiwa ni pamoja na ule wa mwaka 2008 wa kuwajengea uwezo, Midahalo ya rais pamoja na mdahalo wa mchakato wa katiba.



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.