Habari za Punde

Mkutano wa Wadau wa Traffic Plan ya Mji Mkongwe wa Unguja. Kuzuiya Uingiaji wa Magari Stone Town.




Mwenyekiti wa Bodi ya Hifadhi ya Mji Mkongwe wa Zanzibar Bi Mwanaidi Saleh akitowa maelezo kabla ya kuaza kwa mkutano huo wa Wadau wa Mji Mkongwe Zanzibar. 
Waziri wa Ardhi Makaazi na Maji Nishati akifungua mkutano wa Wadau wav Hifadhi ya Mji Mkongwe wa Zanzibar kuzungumzia kupunguza uingiaji wa magari katika mji mkongwe ambao kila siku huiingia magari 17500 kila siku.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Mji Mkongwe Zanzibar Sariboko Makarani akiwasilisha ripoti ya Utafiti wa Uhifadhi wa Mji Mkongwe ili kuweza kuuhifadhi kimataifa ili kuweza kupunguza uingiaji wa magari na kueleza kila siku katika Mji Mkongwe huingia magari 17500.kila siku.

Wajumbe wa Mkutano wa Wadau wa Uhifadhi Mji Mkongwe wa Zanzibar wakifuatilia ripoti wakati ikiwasilishwa na Mkurugenzi wa Masmlaka ya Mji Mkongwe Zanzibar Saliboko Makarani. 
Wajumbe wa Mkutano wa Wadau wea Uhifadhi wa Mji Mkongwe wa Zanzibar wakati wakipitia Trafic Plan ya Mji Mkongwe kuweza kuhifadhi na kuzuiya uingiaji wa magari.  
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bandari Abdalla Juma akichangia wakati wa mkutano huo wa Wadau wa Mjini Mkongwe katika uhifadhi wake kupunguza uingiaji wa magari katika mji mkongwe. 
Mjumbe wa Bodi ya Mji Mkongwe Mhe Simai Mohammed Said akichangia wakati wa mkutano huo wa Wadau wa Mjini Mkongwe Zanzibar.
Mdau kutoka Kameshine ya Utalii Zanzibar Saleh Ferouz akichangia wakati wa Mkutano huo wa Wadau wa kudhibiti uingiaji wa magari katika mji Mkongwe wa Zanzibar.
Wadau wa Traficc Plan ya Mji Mkongwe kuzuiya uingiaji wa magari katika mji mkongwe ili kuweza kuuhifadhi. 
Mdau kutoka Wizara ya Mawasiliano na Miundombinu akichangia wakati swa Mkutano huo wa kudhibiti uingiaji wa Magari katika Mji Mkongwe wa Zanzibar.

1 comment:

  1. Mamlaka ya mji mkongwe ni taasisi inaendeshwa na wataliano kwa hongo. Yote wanayoyazungumza na babaisha bwege tu. ni rushwa, ni rushwa , ni rushwa.Kwa mfano, ndani ya jumba la posta kongwe( jumba class A) katika orodha ya majumba yenye hifadhi ya Mamlaka, ndani kumefungwa generator inayoweza kuendesha kijiji kizima. Likiwasha mtikisiko unaotoa unanyofoa kuta za jengo. Siku moja jumba hili adhimu litaweza kuporomoka. Malalmiko yametolewa lakini hufunikwa kwa (US$)
    Tuwaombe wenye Mamlaka wauhifadhi mji mkonge kwa vitendo

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.