Habari za Punde

Naibu Katibu Mkuu afungua mafunzo ya miezi sita ya ufugaji nyuki , Makunduchi

Naibu  Katibu  Mkuu  wa Habari,  Utalii Michezo na Utamaduni,  ndugu  Issa  Mlingoti amefungua mafunzo ya  miezi  6 ya ufugaji nyuki huko Makunduchi. 

Katika  nasaha  zake amewata wananchi  wa Makunduchi kuhifadhi misitu ili  kuwalinda nyuki.  Aidha amewata washiriki wa mafunzo  hayo kujitahidi kwenye  masomo yao na kuitumia  taaluma watakayoipata kwa vitendo. 

Mafunzo hayo yamefadhiliwa na  bibi Christin Strömberg kutoka Sweden chini ya  mashirikiano kati ya  wadi za Makunduchi na Manispaliti ya  Sundsvall. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.