Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Rashid Ali Juma akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Maonyesho ya kudumu ya sanaa katika maadhimisho ya Makumbusho Duniani yaliyofanyika Makumbusho ya Mnazimmoja Mjini Zanzibar.
Mkuu wa Divisheni ya Makumbusho Zanzibar Khamis Abdalla akimuonyesha Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo sanaa ya ufumaji kofia za asili ya Zanzibar katika maonyesho ya sanaa yanayofanyika makumbusho ya Mnazimmoja.
Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Rashid Ali Juma akiangalia kazi ya ubunifu iliyofanywa na msanii Naaman Ali Khamis wa kwanza (kulia) anaetumia majani makavu ya migomba.
Mkuu wa Divisheni ya Makumbusho kutoka Idara ya Mkumbusho na Mambo ya Kale, Khamis Abdalla akisoma risala ya wafanyakazi wa Idara hiyo katika ufunguzi wa maonyesho ya sanaa ikiwa ni maadhimisho ya siku ya Makumbisho Duniani yaliyofanyika Makumbusho ya Mnazimmoja Zanzibar.
Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Mhe. Rashid Ali Juma akizungumza na wafanyakazi na wananchi walioshiriki maonyesho ya sanaa katika maadhimisho ya ya siku ya Makumbusho Duniani yaliyofanyika Makumbusho ya Mnazimmoja Zanzibar.
Baadhi ya viongozi wa Wizara na wageni waalikwa waliohudhuria ufunguzi wa maonyesho ya sanaa katika maadhimisho ya siku ya Makumbusho Duniani yaliyofanyika Mnazimmoja Mjini Zanzibar wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi.
(Picha na Makame Mshenga/Maelezo)
Na Miza Othman –Maelezo Zanzibar.
Waziri wa Habari, Utalili, Utamaduni na Michezo Zanzibar Rashid Ali Juma amewataka wananchi wa Zanzibar kutumia fursa ya kutembelea Jengo la Makumbusho ya Mnazimmoja ili kuelewa historia ya utamaduni wao .
Waziri Rashid ameyasema hayo katika Sherehe za ufunguzi wa maonesho ya kudumu ya sanaa katika maadhimisho ya siku ya makumbusho dunuani yaliyofanyika Makumbusho ya Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kutoa misaada katika Idara ya Mkumbusho na Mambo ya kale ili isibakie nyuma katika ulimwengu wa sasa ambapo dunia imekuwa kama kijiji.
Waziri wa Habari, Utalii Utamaduni na Michezo amesema wananchi wanahitaji kutunza kumbukumbu na niwajibu kuyatunza maeneo hayo yasipoteze haiba yake ya asili.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utalili, Utamaduni na Michezo Zanzibar Omar Hassan Omar amesema jengo la makumbusho ni muhimu na linapaswa kutuzwa kwani mila, desturi na silka za Zanzibar zinapotea kutokana na kukosekana uhifadhi mzuri.
Aidha ameahidi kushirikiana na wafanyakazi wa Idara hiyo kwa kuwapatia mafunzo ya mara kwa mara ili wawe na uwezo wa kutekeleza kazi zao kwa ufanisi zaidi .
Katika Risala yao iliyosomwa na Mkuu wa Divisheni ya Makumbusho Khamis Abdallah, wafanyakazi hao wamesema wameamua kuandaa maonyesho hayo ya kudumu ya sanaa ili kutoa mwamko na hamasa kwa jamii juu ya upana wa sanaa hiyo.
Wamesema wanajukumu kubwa la kulinda, kuhifadhi na kutunza kumbukumbu za taifa lakini wamekuwa wakikabiliwa na tatizo la maeneo ya kihistoria kuvamiwa na wananchi.
“Tunajikuta tunajukumu kubwa kwa Serikali na hata kwa mwenyenzi mungu kuona kuwa rasilimali hizi zanaanza kupotea zikiwa mikononi mwetu”,alisema Khamiss Abdallah.
Maonyesho hayo yamejumuisha nyanja zote za maisha ikiwemo Mavazi, Ususi, Ufinyanzi, Uhunzi, Uchoraji na Ujenzi ikiwa ni utaratibu mzima wa mfumo wa maisha ya Wazanzibari.
No comments:
Post a Comment