Habari za Punde

Taasisi ya THE SAME QUALITY FOUNDATION wameendesha kambi ya matibabu ya midomo wazi



 Wizara ya afya Zanzibar kwa kushirikian na Taasisi ya THE SAME QUALITY FOUNDATION  wameendesha kambi ya matibabu ya midomo wazi katika hospitali ya mkoa Lumumba ikiwa ni muendelezo wa kambi zinazofanywa na taasisi hio ili kuhakikisha watoto wenye tatizo la midomo wazi wanapatiwa matibabu.

Akizungumza katika kambi hio Mkurugenzi na muazilishi wa Taasisi hio Dr Piter Mabula amesema takriban miaka kumi na moja taasisi hio imekua ikitoa huduma hio na imefanikiwa kufanya  matibabu wa watu zaid ya 2500 kwa Tanzania bara na visiwani ambapo kwa zanzibbar zaid ya watu 200 wamepatiwa huduma hio

Dr.Piter Mabula Mkurugenzi wa taasisi ya THE SAME QUALITY FOUNDATION 

Kwa upande wake Dr Sumaiya Said Abud kutoka katika hospitali ya mkoa Lumumba amesema kambi hio ya siku tano inatarajia kufanya matibabu ya watoto 25 ambao tayar watoto hao wamefanyiwa uchunguzi wa awali

Dr Sumaiya Said Abud hospitali ya mkoa Lumumba

Sambamba na hayo sumaiya ametoa wito kwa wazazi na walezi wenye watoto wenye tatizo la mdomo wazi kuwafiikisha katika hospitali hio  ili kupatiwa matibabu

CLIP… Dr Sumaiya Said Abud hospitali ya mkoa Lumumba

Nao wazazi wa watoto waliopatiwa huduma hio wameishukuru serikali ya mapinduzi ya Zanzibar pamoja na taasisi ya THE SAME QUALITY FOUNDATION kwa kuwapatia huduma hio bure hali ambayo inawapa faraja ya watoto wao,

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.