Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein(katikati waliokaa) akiwa katika Picha ya Pamoja iliyowajumuisha Viongozi mbali mbali baada ya kuapishwa kwa watendaji wa Serikali ya Mapinduzi katika Wizara tofauti
[Picha na Ikulu.]{28/06/2016.
STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 28.6.2016
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amewapisha viongozi mbali mbali kushika nyadhifa
katika taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Walioapishwa ni Dk.
Islam Seif Salim kuwa Naibu Katibu Mkuu, Mifugo na Uvuvi katika Wizara ya
Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi ambapo kabla ya wadhifa huo alikuwa Naibu
Katibu Mkuu iliyokuwa Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
Hassan Abdulla Mitawi ameapishwa
kuwa Naibu Katibu Mkuu, Habari katika Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na
Michezo ambapo kabla ya wadhifa huo alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habari
la Zanzibar (ZBC).
Aidha, Dk. Shein
amemuapisha Rafii Haji Makame kuwa Katibu Mtendaji Tume ya Utangazaji Zanzibar katika Wizara ya Habari,
Utalii, Utamaduni na Michezo ambapo kabla ya wadhifa huo alikuwa Mkurugenzi wa
Idara ya Habari Maelezo katika Wizara hiyo.
Hafla ya kuwaapisha viongozi
hao ilifanyika Ikulu Mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar akiwemo Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir
Ali Maulid, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa
Haji Gavu, Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Rashid Ali Juma.
Viongozi wengine ni na
Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Hamad Rashid, Naibu Waziri wa
Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Chumu Kombo Khamis, Mwanasheria Mkuu wa
Zanzibar Said Hassan Said, Katibu Mkuu Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Salum Maulid Salum.
Wengine ni Kadhi Mkuu
wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji, Mkuu wa
Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud, Meya wa Manispaa ya Mji
wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib pamoja na Washauri wa Rais wa Zanzibar na
viongozi wengine wa Serikali.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment