Habari za Punde

Wafanyabiashara Pemba washangazwa na mabadiliko ya ghafla ya kupandisha kodi


Na salmin Juma –Pemba

Wafanyabiashara wa soko la Chakechake mkoa wa kusini Pemba wamedai  kustaajabishwa na mageuzi ya ghafla yaliyofanywa na baraza la mji wa Chakechake kwa kuwapandishia bei ya gharama za ulipaji kodi kwa 100% pamoja na upunguzaji wa vikuta  vya biashara.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti baadhi ya wafanyabiashara wa maeneo hayo wameelezea  masikitiko yao   kwa kusema kua, hali ya maisha kipindi hiki ni ngumu mno kwa wakaazi wa  kisiwani humo na wanavyofanyiwa na  baraza la mji kwa kupandishiwa kodi  kwa kiwango cha juu ni sawa na kuwakomoa .

Mmoja miongoni mwa wafanyabiashara sokoni hapo   bw: Rashid Ali Zaina  amesema kua uwamuzi uliyochukuliwa na baraza la manispaa la mji huo ni  jambo la ajabu kwao akisema kua awali waliendesha biashara zao katika mazingira yaliokua afadhali wakati kikuta kimoja walikilipia Tsh 20,000/= kwa mwezi  lakini sasa wametakiwa kukilipia  Tsh 50,000/=  hali aliyodai kua inawapa ugumu na kuwaumiza  ukilinganisha na mwenendo wa biashara zenyewe sokoni hapo.

Amesema awali kikuta kimoja alichokua nacho sasa kimekatwa na kua vikuta viwili na kila kimoja kinatakiwa kulipiwa gharama hiyo huku akisema kua icho kimoja hakitoshelezi kuwekea bidhaa zao kutokana na udogo wake.

 “kwakweli hali ni ngumu kwasababu hii sehemu niliyoachiwa hata kama nauza samaki haitoshelezi wakati nna biashara karibu kumi au kuminatano zote zinataka kupangwa katika eneo hili, sasa utakuta nipo katika hali ngumu sitaweza hata kufanya lolote katika eneo hili na wanafanya hivi kwakutukomoa kisiasa na kwakweli uwongozi huu wa baraza la mji wote hautufai kwa sababu ni watu waliyopandikizwa kisiasa kutukomoa sisi wapemba”alisema Zaina.


Katibu wa soko bw: Ali Muhammed Salim  amesema kukatwa kwa  vikuta hivyo ni uwonevu wanaotendewa na ni jambo linalo muuma sana kuliko hata wafanyabiashara wengine.

Amesema sokoni hapo wanauowongizi wao wafanyabiashara lakini wanauwona hauna nafasi  katika jambo lolote kwa baraza la mji  kwa sababu hakuna wanalotatuliwa katika wanayoyasema kama changamoto kwao.

“Uwongizi wetu hauna nafasi yoyote kwa baraza hili kwa sababu kama tuna nafasi madai yetu yangekua yanasikilizwa ingawa tunaitwa na tunawaelezea lakini hayatekelezwi na si hili tu kuna mengi tushayaongelea, kuna tatizo la vyoo, kama unavyosikia ndugu mwandishi  maradhi ya mripuko yaliyomo visiwani mwetu, tuliomba kurekebishiwa tatizo hilo lakini hatukutekelezewa, tunaukosefu wa maji lakini hakuna kilichofanyika mpaka leo”alisema Katibu huyo.

Nae mfanyabiashara wa mazao ya mbogamboga sokoni hapo ambae hakupenda jina lake liandikwe amemwambia mwandishi wa habari hii kua kodi iliyozidishwa inawapa wakati mgumu kukabiliana na ukali wa maisha akisema haiwezekani kodi kupandishwa kutoka Tsh 20,000/= mpaka  Tsh 50,000/= ukizingatia mkataba haukusema hivyo.

Amesema hakuna mfanyabiashara anaepinga kulipia kiasi hicho lakini sikuzote mambo huwenda kwa maafikiano baina ya wahusika wa pande mbili tofauti na ilivyofanywa na baraza hilo kuwapadishia kodi kinyume na mkataba waliofungiana.


Akizungumzia suala la ukatwaji wa vikuta sokoni hapo  ameungana na wafanyabiashara wengine kwa kusema kua , ukubwa wa vikuta walivyokua wakivimiliki mwazo sasa vimepunguzwa hali ambayo amesema inawapashida pakuziweka bidhaa zao.


(salminjsalmin@gmail.com)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.