Habari za Punde

Utalii wa ndani: Wanafunzi wa Skuli ya Sekondari Madungu watembelea msitu wa hifadhi ya Ngezi Makangale

 MTEMBEZA wageni katika msitu wa hifadhi ya Ngezi Makangale Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kusini Pemba, Mohamed Khalfan Massoud akitoa historia ya Msitu huo, kwa wanafunzi wa skuli ya Sekondari Madungu Chake Chake Pemba, wakati walipofanya ziara ya kitalii katika msitu huo wakiongozwa na Kamisheni ya Utalii Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA).
 WANAFUNZI wa Skuli ya Sekondari Madungu Chake Chake Pemba, wakimsikiliza mtembeza wageni katika msitu wa Ngezi Makangale Mohamed Khalfan Massoud, wakati alipokuwa akiwafahamisha aina za misitu iliyomo ndani ya Msitu huo.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA).
 MTEMBEZA wageni katika msitu wa Hifadhi wa Ngezi Makangale Mohamed Khalfan Massoud, akiwaonyesha wanafunzi wa skuli ya Sekondari Madungu mabaki ya viwanda vya kupasualia mbao, kilichokuwa kikifanya kazi ndani ya msitu wa ngezi katika kipindi cha wakoloni.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA).
 MMOJA wa ina ya ndege adimu Zanzibar anayejulikana kwa jina la Kidonati, ndege huyu anadaiwa kutoa nchini Madagaska na hupatikana katika msitu wa ngezi Kisiwani Pemba katika mwezi wa Septemba na Januari.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA).
 MWANDISHI wa Habari wa ZBC TV kisiwani Pemba, Nassra Mohamed Khatib akichukuwa baadhi ya maelezo ya mmoja wa ndege adimu anayepatikana katika msitu wa ngezi Kisiwani Pemba, Kidonati ndege huyo anadaiwa kutoka nchini Madagaska.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.