Habari za Punde

Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Dk Mahadhi Maalim akutana na katibu Mkuu baraza la Taifa la Sanaa na utamaduni la Kuwait




Mhe. Dkt. Mahadhi J. Maalim, akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Ali Al-Yoha, Katibu Mkuu, Baraza la Taifa la Sanaa na Utamaduni la Kuwait.



 Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim,, amemtembelea Mhe. Ali Al-Yoha, Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa na Utamaduni la Kuwait ofisini kwake tarehe 04 Septemba 2016.

 
Katika ziara hiyo, Mhe. Dkt. Maalim alipata fursa ya kufanya mazungumzo na Mhe. Al-Yoha kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Kuwait katika eneo la Sanaa na Utamaduni. Mhe. Al-Yoha, alimhakikishia Mhe. Maalim kuwa Kuwait ipo tayari kufanikisha ushiriki wa Tanzania katika matamasha mbalimbali ya Sanaa na Utamaduni yanayoandaliwa na Baraza hilo.

 

Kwa upande wake, Mhe. Dkt. Maalim, alimshukuru Katibu Mkuu huyo na kumuahidi kuwa Ubalozi wa Tanzania nchini Kuwait upo tayari kuratibu zoezi hilo la upatikanaji wa vikundi vya utamaduni na sanaa kutoka Tanzania ili viweze kushiriki katika matamasha hayo kwa lengo la kutangaza utamaduni na sanaa ya Tanzania.

 

Kadhalika, Mhe. Maalim alisisitiza kuwa pamoja na mambo mengine, eneo hilo la Sanaa na Utamaduni ni muhimu sana katika kukuza mahusiano na maelewano ya watu wa pande hizi mbili.

 

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.