STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Pemba 11.9.2016
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amepokea kwa masikitiko
makubwa taarifa ya vifo na maafa mengine vilivyotokana na tetemeko la ardhi
lililotokea jana Septemba 10, 2016 majira ya laasiri katika Mkoa wa Kagera
pamoja na maeneo mengine ya jirani.
Kufuatia
tukio hilo Rais wa Zanzibar anaungana na familia zote zilizopoteza ndugu, jamaa
na marafiki na anawaombea marehemu wapumzishwe mahala pema panapostahiki na awape subira ndugu, jamaa na
marafiki wa marehemu hao katika kipindi hiki kigumu.
Aidha,
Dk. Shein amewaombea kwa Mwenyezi Mungu majeruhi wote walioathirika kutokana na
tetemeko hilo wapone haraka na kurejea katika hali zao za kawaida ili waweze
kufanya shughuli zao za kila siku kwa manufaa yao na taifa kwa jumla.
Wananchi
wa Zanzibar wanaungana Mkuu wa Mkoa wa
Kagera, wananchi wake pamoja na Watanzania wote kwa jumla katika kuomboleza
msiba huo.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment