Habari za Punde

Wavuvi Chwaka wapiga hatua kudhibiti uvuvi haramu

Na Fatma Makame MCC  21/09/2016.

Wavuvi wa kijiji cha Chwaka wamepiga hatua ya kuweza kudhibiti uvuvi haramu kijijini humo kwa lengo la kuleta maendeleo ya uvuvi .

Kauli hiyo imeetolewa na wananchi wa kijiji hicho wakati wakizungumza na Mwandishi wa habari hizi, walisema kudhibitiwa  kwa uvuvi haramu kijijini humo kumetokana na mashirikiano makubwa baina  ya wananchi na wavuvi.

Walisema mafanikio hayo yametokana na  kuunda  kwa kamati ya uvuvi yenye lengo la kuwasimamia  shughuli  zote za bahari pamoja na kufuata maelekezo yanayotolewa na Idara ya Uvuvi.

“Kuundwa kwa kamati hiyo kumeweza kutatua matatizo mengi yanayotokana na uvuvi haramu na hasa pale  yanapotokea maafa baharini,”walieleza

Hata hivyo wameeleza kuwa Kamati hiyo imeweka mikakati kwa mvuvi yeyote atakae kwenda kinyume na taratibu ziliwekwa atachukuliwa hatua za kisheria.

Aidha walifahamisha kuwa wavuvi wa kijiji hicho wanatarajia kupata msaada wa meli kupitia  Idara ya uvuvi ambayo  wataweza kuvua masafa ya mbali ili kuondokana  na migongano na wavuvi wadogo wadogo  .

Nao Wavuvi hao walisema kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni uingiaji wa  meli kutoka nje ya nchi kuja kuvua kijijini hapo jambo ambalo linapelekea  kukosa mafanikio katika kazi yao hiyo na kurudi nyuma  kimaisha.

Pia wananchi hao wamewataka vijana kujishughulisha na kazi za kujipatia maendeleo ili kuepukana na vitendo viovu ambavyo havistahiki katika jamii .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.