Habari za Punde

Wizi wa mifugo wakithiri Dunga,warudisha nyuma maendeleo

Na Fatma Makame MCC              21/9/2016

Wananchi  wa kijiji  cha  Dunga kiembeni wameliomba Jeshi la Polisi kufuatilia tatizo la wizi wa mifugo jambo ambalo linawarudisha nyuma  kimaendeleo .

Akizungumza  na waandishi wa habari hizi Ali Juma Salum  amesema  tatizo hilo limekithiri kijijini hapo kwani hupelekea wafugaji kuvunjika moyo kutokana  na  kupungua idadi ya mifugo yao .

Alisema  wizi huo unatokana na vijana  wengi kutojishughulisha na kazi  za mikono za  kujipatia kipato cha kuweza  kijikimu kimaisha jambo ambalo linachangia kuzorotesha maendeleo .

“Vijana wanapenda kutumia  bila kujishughulisha na kazi yeyote hatimae kujiingiza katika vitendo vya wizi wa mifugo”alisema Ali Juma.

Aidha alisema wafugaji wengi wanakata tamaa kutokana na wizi wa mifugo mbali mbali ikiwemo  n’gombe, mbuzi ,kuku, pamoja na  bata jambo ambalo linawatia hasara katika ufugaji wao .

Nae Mjumbe  wa Sheha wa Shehia hiyo Kesi Makame Mussa  amekiri kuwepo kwa vitendo hivyo na kuwataka wananchi waendelee na ufugaji  na tatizo hilo litatafutiwa ufumbuzi .

Hata hivyo sheha huyo amesema atahakikisha anashirikiana na Jeshi la Polisi  ili kupunguza vitendo hivyo katika kijiji hicho.

Sambamba na hayo amewata wananchi wawe na mashirikiano ili kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa .                                                                           
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
   

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.