Habari za Punde

Waziri Ali Karume ziarani Pemba kukagua miradi ya maendeleo

 WAZIRI wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar Mhe:Balozi Ali Abeid Karume, akikagua barabara ya Ole-Kengeja eneo la Mfikiwa,eneo ambalo udongo wake umelazimika kutolewa na kufukiwa fusi kulia ni Injinia Amini Khalid Abdalla anaesimamia barabara hiyo.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 AFISA Mdhamini Wilara za Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Pemba, Hamad Ahmed Mohamed (Baucha) kushoto akimpatia maelezo Waziri wa Wizara hiyo Mhe:Balozi Ali Abeid Karume, wakati wa ziara yake ya kukagua barabara ya Ole-Kengeja Kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WAFANYAKAZI wa barabara ya Ole-Kengeja wakiwa katika kuchukua taarifa mbali mbali baada ya kukalisha vipimo vyao, kama walivyokutwa wakipima baraabra hiyo katika eneo la Vitongoji.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WAZIRI wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar, Mhe:Balozi Ali Abeid Karume, akimuelezea jambo Injinia Mkaazi wa Wizara yake Pemba, Rashid Said wakati waziri huyo alipokuwa akikagua barabara ya Mgagadu-Kiwani ambayo kwa sasa iko katika kiwango cha Lami.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WAZIRI wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar, Mhe:Balozi Ali Abeid Karume, akikagua ukumbi utakaoweza kufanyika sala ya Eid el hajj, mwaka huu huko Mkanyageni Wilaya ya Mkoani Kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WAZIRI wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar, Mhe:Ali Abeid Karume akipata maelezo ya Ukumbi utakaofanyika baraza la Eid llhaji mwaka huu, huko Mkanyageni Wilaya ya Mkoani, kushoto ni injinia Vekaria Mvrji kutoka kampuni ya Rans Consultation LTD Zanzibar.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 AFISA Mdhamini Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Pemba, Hamad Ahmed Mohamed (Baucha), akimpatia maelezo waziri wa Wizara hiyo Mhe:Balozi Ali Abeid Karume, wakati alipotembelea kukagua eneo litakalo fanyika swala ya Eid ll Haj mwaka huu huko bandarini Mkoani.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WAZIRI wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar, Mhe:Balozi Ali Abeid Karume akizungumza na Ali Omnar Khamis mmoja wa wakaazi wa nyumba za Maendeleo Kengeja, wakati wa ziara yake ya kuangalia maendeleo ya Nyumba hizo.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WAZIRI wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar, Mhe:Balozi Ali Abeid Karume akiteremka chini baada ya kukagua nyumba za maendeleo Kengeja Mkoani.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 BAADHI ya maeneo ya nyumba za maendeleo Kengeja yakiwa katika hali mbaya kama yanavyoonekana katika picha, nyumba hizo zilijengwa na Marehemu Rais wa kwanza wa Zanzibar Abeid Amani Karume kwa ajili ya wananchi.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
WAZIRI wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar, Mhe:Balozi Ali Abeid Karume, akimfahamisha jambo Afisa Mdhamini wa Wizara hiyo Pemba, Hamad Ahmed Mohamed Baucha wakati walipokuwa wakikagua nyumba za maendeleo Kengeja Mkoani.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

1 comment:

  1. Maendeleo ni kusonga mbele, lakini hizo nyumba za maendeleo naona zinarudi nyuma

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.