Habari za Punde

Nauli za ATCL kuanzia Oktoba14 hadi 28

atc-2
atc-2
Ndege mbili mpya za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) aina ya Bombardier Q400 zinatarajia kuanza kazi wakazi wa mikoa ya Mwanza, Arusha na Zanzibar watakuwa wa kwanza kupata ofa.
Ofisa Habari wa shirika hilo, Lilian Fungamtama amesema safari mpya za ndege hizo ikiwamo ya Dar es Salaam – Mwanza, nauli iliyopangwa ni Sh160,000.
Amesema safari za Dar es Salaam – Arusha nauli yake itakuwa Sh180,00 na Zanzibar – Dar es Salaam ni Sh85,000.
“Ofa hii imetolewa na ATCL kwa safari mpya za ndege hizo,” alisema Fungamtama.
Amesema hakutakuwa na safari ya moja kwa moja kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar, lakini itakuwapo ya kutoka Dar es Salaam -Arusha hadi Zanzibar.
“Ndege ya kutoka Dar es Salaam kwenda Arusha ndiyo itakayokwenda kuchukua abiria Zanzibar haitatokea Dar es Salaam moja kwa moja,” alisema.
Akifafanua kuhusu nauli hizo, Fungamtama alisema nauli ya kutoka Dar kwenda Kigoma itakuwa katika madaraja mawili ambayo ilikuwapo tangu awali.
Amesema bado ndege hizo hazijaanza safari katika mikoa yote hadi hapo watakapotangaza.
Akizungumzia safari za nje ya nchi, alisema itakuwapo ya kutoka Dar es Salaam – Hahaya hadi Comorro ambayo nauli yake ni Sh543,950 kwenda na Sh926,650 kwa kwenda na kurudi.
“Lengo letu ni kutoa huduma nzuri itakayomridhisha kila mteja,” alisema Fungamtama.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.