Habari za Punde

Wananchi Kisiiwani Pemba Watakiwa Kutembelea Maeneo ya Utalii Kuimarisha Utalii wa Ndani Nchini.

Na Salmin .J. Salmin Pemba.
Jamii imeshauriwa kuuthamini  utalii wa ndani ikiwa ni njia moja wapo ya kuwasaidia kujikwamua kiuchumi na  kuitambua historia ya nchi yao

Mdahamini wa kamisheni ya Utalii Pemba Maalim Suleiman Amour Suleiman amesema endapo jamii itakuwa na utamaduni wa kuyatembelea maeneo hayo itapata fursa ya kuelewa mambo mbalimbali ya kihistoria na kuyaenzi kama kivutio kwa wageni

Hayo ameyasema huko Ras Mkumbuu alipokuwa katika ziara ya kuyatembelea magofu hayo na kubuni  mikakati itakayosaidia  kuyalinda ili kutopoteza  haiba yake.

Naye msimamizi wa magofu ya Mkumbuu Rashid Ali Said amesema mbali na changamoto wanazokabiliana nazo katika kuyahifadhi maeneo hayo kutokana na uharibifu wa kimazingira lakini ufahamu mdogo  wa wananchi  juu ya kuyaenzi magofu hayo bado unarejesha nyuma ustawi wa magofu hayo.

Amesema katika kuyatangaza magofu ya Mkumbuu kiutalii huwaalika wananchi na wanafunzi kutoka skuli mbalimbali kutembelea na kujifunza historia ya mambo ya kale.

Magofu hayo ya Ras Mkumbuu ambayo yamevumbuliwa tokea karne ya tisa yamekuwa kivutizi kikuu cha utalii kutokana na historia yake ya kuwa na msikiti wakale  na kaburi la  mwanamwari.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.