Na Daudi Manongi. Maelezo Dae es Salaam.
Bagamoyo
WAZIRI wa
Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Mhe.Jenista
Mhagama amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Bw.Majid Mwanga kuhakikisha ana
tatua mgogoro wa  ujenzi wa barabara ya Kiwangwa-Mabohelo  yenye
urefu wa kilomita 15 na kumalizika mwishoni mwa mwezi huu.
Ameyasema
hayo jana Wilayani  wakati alipotembelea  miradi inayotekelezwa na
Halmashauri  ya Wilaya ya Chalinze na
Bagamoyo  kwa ufadhili wa Programu ya  Miundombinu ya  Masoko, Uongezaji
Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini(MIVARF)  inayosimamiwa na chini ya
Ofisi ya Waziri Mkuu.
“Serikali
ya Awamu ya Tano ina lengo kubwa la kuwasaidia wananchi hususani wakulima ili wafikiwe
na miundombinu ili kupambana na umaskini na kuboresha masuala ya masoko yao na
hivyo kuwaongezea kipato”, Alisema Mhagama.
Aidha
Mhe. Mhagama alisema kuwa asili ya miradi ya ufadhili wa Programu ya Miundombinu
ya  Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF) iliyo
 chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu haina fidia hivyo  anashangaa kuona ni
kwanini ujenzi vipande hivyo vitatu vya barabara vinachelewa kukamilika hadi
kufikia leo.
Ameongeza
kuwa pesa za kumalizia mradi huo zipo na kusema kuwa tatizo kubwa lililopo ni
kukosekana kwa mawasiliano kati ya Halmshauri za Bagamoyo na Chalinze na
kuwaagiza Viongozi wa Halmashauri hizo chini na kumaliza mgogoro huu mara moja
ili  wananchi wafanikishe lengo kuu la mradi huo ambao ni umwagiliaji.
Kwa
upande wake Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mhe.Ridhiwani Kikwete alisema kuwa
tatizo kubwa  linalofanya mradi huo kutokamilika ni kutoshirikishwa kwa
wananchi  na kuitaka halmashauri ya Bagamoyo kukaa pamoja na wao ili
kupata ufumbuzi wa kudumu.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo
Bw.Majid Hemed Mwanga aliahidi kulipatia ufumbuzi tatizo la mgogoro huo ndani
ya muda alioagizwa  kwa kuwashirikisha madiwani wote.

No comments:
Post a Comment