Habari za Punde

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Ndg. Shaka Hamdu Azungumza na Watumishi wa UVCCM Makao Makuu leo.

Kaimu Katibu Mkuu Uvccm Shaka Hamdu Shaka  akizungumza na watumishi wa UVCCM  Makao Makuu   kutathmini utendaji wa jumuiya kwa mwaka 2016 na kupanga mikakati ya mwaka 2017 pamoja na kusikiliza michango  mawazo na changamoto mbali mbali zinazowakabili watumishi hao na namna ya kuzitatua ili mwaka 2017 uwe wa mafanikio zaidi.
''Tuongeze bidii ya kazi kila mmoja katika nafasi yake nilazima afahamu na kutambua ya kwamba kila mfanyakazi wa jumuiya katika eneo lake, mchango wake na juhudi za zake zinahitajika sana hasa katika hichi kipindi cha kuleta mageuzi makubwa ya kiutendaji kwa wanachama wetu ''Alisema  Kaimu Katibu Mkuu Uvccm Shaka Hamdu Shaka wa kwanza kushoto akizungumza na watumishi wa UVCC Makao Makuu  Upanga Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Utawala UVCCM Ndg:Omary Ng'wanang'walu liposimama kuzungumza katika kikao hicho cha   kutathmini utendaji wa jumuiya kwa mwaka 2016 na kupanga mikakati ya mwaka 2017 leo Makao Makuu  UVCCM Upanga Dar es Salaam .
Kaimu Mkuu wa Idara ya Hamasa,Sera,Utafiti na Mawasiliano Ndg:Mtemi Sylvester Yaredi akizungumzia juu ya Mikakati ya Maswala Mbalimbali katika idara yake katika kikao hicho cha   kutathmini utendaji wa jumuiya kwa mwaka 2016 na kupanga mikakati ya mwaka 2017 leo Makao Makuu  UVCCM Upanga Dar es Salaam .
Kaimu Mkuu wa Idara ya Uchumi na Fedha Bi:Tumain Mwakasege akizungumzia juu ya Mikakati  Mbalimbali katika idara yake katika kikao hicho cha kutathmini utendaji wa jumuiya kwa mwaka 2016 na kupanga mikakati ya mwaka 2017 leo Makao Makuu  UVCCM Upanga Dar es Salaam
Mtumishi Wa Makao Makuu UVCCM Ndg:Pamphil James Hwago wa kwanza kushoto  akimuelezea Kaimu Katibu Mkuu Shaka wa kwanza kuli juu ya changamoto  za maswala mbali mbali yanayowakabili Watumishi Makao Makuu  UVCCM Upanga Dar es Salaam leo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.