Habari za Punde

Naibu Waziri Mhe.Kigwangalla Awakabidhi Kadi za Bima ya Afya Wazee 200 wa Jimbo la Kikwajuni Zanzibar.

Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akimkaribisha Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala, katika Sherehe za Kukabidhi Bima ya Afya kwa Wazee wa Jimbo la Kikwajuni, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnarani, MwembeKisonge, MjiniUnguja, Zanzibar. 

Naibu  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala akizungumza na wananchi wa Jimbo la Kikwajuni (hawapopichani), kabla ya kukabidhi kadi za Bima ya Afya kwa wazee zaidi ya 200 wa jimbo hilo ambalo anatoka Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni (kushoto). Kulia ni Mwakilishi wa Jimbo hilo,Mhe. Nassor Salim Jazeera. Tukio hilo lilifanyika katika Viwanja vya Mnarani, MwembeKisonge, Mjini Unguja, 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala, akimkabidhi Bi. Salma Salum kadi ya bima ya Afya katika viwanja vya Mnara wa Michezani MwembeKisonge, Mjini Unguja, Zanzibar. Kadi zaidi ya 200 walikabidhiwa wazee wa Jimbo la Kikwajuni la Mhe Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na wananchi wakati wa hafa hiyo ya kukabidhi Kadi za Bima ya Afya kwa Wazee wa Jimbo la Kikwajuni Zanzibar jumla ya wazee 200 wamefaidia na mchango huo wa Mbunge na Mwakilishi kupata matibabu bure kwa kutumia kadi hizo. Hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya mnara wa kumbukumbu michezani kisonge. 
 Naibu Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapindiuzi, Zanzibar, Mhe.Harusi Said akizungumza na wananchi katika Sherehe za kukabidhi Bima ya Afya kwa Wazee zaidi ya 200 wa Jimbo la Kikwajuni, zilizotolewa na Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo hilo hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Mnara wa Michezani Zanzibar. MwembeKisonge, MjiniUnguja, Zanzibar.  Pichana Felix Mwagara.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.