STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 13.2.2017
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amesema kuwa Tume zote duniani zina majengo na ofisi
zinazofanana na hadhi na kazi zinazofanywa na ofisi hizo hivyo, Serikali
anayoiongoza itahakikisha Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) inapata ofisi
zinazokwenda na wakati kabla ya uchaguzi ujao wa mwaka 2020.
Dk. Shein aliyasema hayo
leo mara baada ya kufanya ziara fupi ya kulitembelea jengo la Ofisi za Tume ya
Uchaguzi ya Zanzibar huko Maisara mjini Zanzibar, ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa
hivi karibuni wakati alipokabidhiwa ripoti ya uchaguzi wa tarehe 25 Oktoba
pamoja na uchaguzi wa Marudio wa tarehe 20 Machi 2016 na Mwenyekiti wa Tume ya
Uchaguzi ya Zanzibar Jecha Salim Jecha kuwa leo atazitembelea Ofisi hizo.
Katika maelezo yake
Dk. Shein alisema kuwa Tume zote za uchaguzi
duniani zipo katika mazingira na
sehemu nzuri kwa kutambua kuwa chombo kinachosimamia uchaguzi ni lazima kiwe
katika mazingira mazuri yanayoendana na hadhi yake hivyo, lazima Serikali
ifanye juhudi za kuhakikisha Ofisi za Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar inakuwa
katika mazingira mazuri.
Dk. Shein alisema kuwa
ni vyema wakati uchaguzi wa mwaka 2020 ukiandaliwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar
(ZEC) iwe na Ofisi nzuri na zenye nafasi kwa ajili ya kufanya kazi zao kwa
ufanisi zaidi pamoja na vifaaa na vitendea kazi imara yakiwemo magari na
kuahidi kuwa Serikali anayoiongoza itafanya juhudi katika kuhakikisha
changamoto hiyo inapata ufumbuzi.
Alisema kuwa kwa
upande wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) tayari inampango wa kujenga jengo
lake huko Dodoma ambalo litakuwa na mazingiza mazuri hivyo, kwa upande wa
Zanzibar Ofisi hizo za Tume nazo ni vyema zikawa zinaenda na wakati uliopo kwa
kuwa na majengo yanayoendana na hadhi ya Tume.
Kutokana na hilo, Dk.
Shein aliahidi suala hilo kupatiwa ufumbuzi na jawabu muwafaka litapatikana haraka
iwezekanavyo na kusema kuwa wakati wowote jibu muwafaka litapatikana kama
Serikali itajenga jengo jipya ama kufanyiwa ukarabati au upanuzi kwa majengo
yaliopo sehemu hiyo likiwemo jengo jengine pembezoni mwa Ofisi za Tume hizo
ambalo halitumiki kwa sasa.
“Nitafanya maamuzi leo
na mchana huu tutakuwa na kikao na tutaamua na kukuarifuni maamuazi tuliyoamua
juu ya ujezi wa Ofisi ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar”,alisisistiza Dk. Shein.
Aidha, Dk. Shein
alielendelea kuwasisitiza viongozi na wafanyakazi wa Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar waendelee kufanya kazi zao na kujituma huku akiwaahidi kuwa Serikali
yao ya Mapinduzi ya Zanzibar ipo na itaendelea kuwaunga mkono na wala wasiwe na
wasi wasi.
Mapema Mwenyekiti wa
Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Jecha Salim Jecha
alitoa pongezi zake kwa niaba ya Tume hiyo kwa Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein kwa kufanya ziara yake
hiyo ya kuzitembelea Ofisi za Tume hiyo kutokana na ombi lake alilolitoa kwa
Rais hivi karibuni.
Mwenyekiti huyo wa
Tume ya Uchaguzi alitumia fursa hiyo kueleza changamoto wanazozipata kutokana
na ufinyu wa nafasi katika ofisi zao sambamba na mahitaji yao ya vifaa na
vitendea kazi vyengine yakiwemo magari.
Katika ziara hiyo Dk.
Shein alitembelea sehemu mbali mbali za ofisi hiyo na kupata maelezo kutokana
na changamoto ya ufinyu wa nafasi za ofisi za Tume hiyo, pia, alioneshwa
kiwanja kiliopo pembeni ya jengo la Tume hiyo pamoja na kukagua, jengo ambalo
halitumiki kwa hivi sasa ambalo liko pembezoni mwa ofisi za Tume hiyo.
Viongozi mbali mbali wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, waliungana na Rais Dk. Shein katika ziara
hiyo fupi ambayo pia, ni muhimu akiwemo Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar,
Balozi Seif Ali Idd, Mawaziri, Makamishna na viongozi wengine wa Serikali.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment