Na Salmin Juma, Pemba
Walimu wanaosomesha Vituo vya Mafunzo ya Amali Kisiwani Pemba wametakiwa kuyatumia vyema mafunzo walioyapata ili yaweza kufanikisha malengo yaliokusudiwa.
Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji kutoka Mamlaka ya Mafunzo ya Amali Zanzibar Bakari Khamis Juma wakati alipokwa akifungua mafunzo ya siku tano huko katika ukumbi wa kituo cha Amali vitongoji Chake Chake Pemba.
Amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo walimu wa vituo hivyo na kuwa wabunifu ili nao wakawaendeleze vijana mbinu mbali mbali za kuzalisha miradi itakayopelekea kuapatia kipato na kuondokana na hali ngumu za maisha.
Aidha Mkurugenzi huyo ameitaka jamii kuwapeleka vijana wao waliomaliza masomo ya darasa la kumi katika vituo vya Elimu Mbadala ili waweze kujiendeleza na shughuli mbali mbali za ujasiriamali na kuweza kujiajiri wenyewe.
Kwa upande wa wawezeshaji wa mafunzo hayo wamewataka walimu hao kusikiliza kwa makini mbinu za ubunifu na uvumbuzi wa miradi ili wawe walimu wazuri wanapo wafundisha vijana namna ya kuzalisha miradi hiyo.
Nao washiriki wa mafunzo hayo wametowa wito kwa jamii kuwapeleka vijana wao katika vituo hiyvo kwa ajili ya kujiendeleza kitaaluma zaidi na kujiepusha na vitendo viovu ndani ya jamii zao.
No comments:
Post a Comment