Naibu Waziri Ofisi ya Makamo wa Rais Muungano na Mazingira wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Luhaga Joelson Mpina,akishiriki katika ujenzi wa bwawa la kuvunia maji ya Mvua linalojengwa kwa ufadhili kupitia mfuko wa maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF 3) huko katika Shehia ya Kibokoni Vitongoji Pemba.
Naibu Waziri Ofisi ya makamo wa Rais Muungano na Mazingira wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Luhaga Joelson Mpina, akizungumza na mjenzi wa Soko hilo la konde Pemba,mara baada ya kuangalia maendeleo ya Ujenzi wa Soko la Konde Wilaya ya Micheweni linalojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa MIVARF.
Mkuu wa Wilaya ya Micheweni, Abeid Juma Ali, akizungumza na Naibu Waziri Ofisi ya makamo wa Rais Muungano na Mazingira wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Luhaga Joelson Mpina, mara baada ya kuangalia maendeleo ya Ujenzi wa Soko la Konde Wilaya ya Micheweni linalojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa MIVARF.
(Picha na Habiba Zarali - Pemba)
No comments:
Post a Comment