Na
Abdi Shamnah
KUWEPO
kwa usafiri wa ndege ya Abiria ya Airbus A350 kutoka Shirika la Ethiopian
Airlines, na kuunganisha safari zake
hadi Zanzibar, kutapanua wigo wa ujio wa watali nchini.
Ndege
hiyo mpya yenye uwezo wa kuchukua abiria 345, iliyoundwa kwa teknolojia ya juu
zaidi, ni ya kwanza Barani Afrika,
ambapo kwa mara ya kwanza imewasili
katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume, jana ikitokea mjini
Addis Ababa, Ethiopia – Kilimanjaro – Zanzibar.
Lengo
la safari hiyo, ni kuitangaza ndege hiyo, ikiaminika itakuwa na mchango mkubwa
katika uimarishaji wa sekta ya utalii nchini.
Akizungumza
mara baada ya kuwasili kwa ndege hiyo, Meneja Mauzo na wakala wa huduma, Tawi
la Zanzibar, Mohammed Mansour, alisema watalii wengi duniani wanapenda kusafiri na mashirika ya
ndeeg yenye uhakika na usalama wa safari.
Alisema
kuja kwa ndege hiyo kutawahamaisha watalii duniani kote, kufika Zanzibar na
kutembelea vivutio mbali mbali vya utalii viliopo.
Mapema
Meneja wa Masoko wa Ethiopian Airlines, Eshetu Fikadu alisema ndege ya A350
imetengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu zaidi, ikikidhi viwango vyote na
yenye kuleta faraja kwa marubani, wafanayakazi pamoja na abiria wakati wa
safari.
Alisema
Shirika la Ethiopian Airline limekuwa likitowa huduma zake kwa zaidi ya nusu karne sasa Barani Afrika,
na kuyafikia maneo mbali mbali, ikiwemo yale yenye vivutio vya utalii.
Alisema
kuwepo kwa ndege hiyo, ambapo safari zake nchini zinategemea na mahitaji yatakavyokuwa,
kutawafanya watalii kutoka mataifa mbali mbali barani Ulaya na Mashariki mbali,
kuunganishwa na ndege hiyo na kuzuru
Zanzibar.
Ndege
ya A350, ina uwezo wa kuchukua abiria
315 wa daraja la kawaida (Economy) pamoja na abiria 30 wa daraja la kwanza.
No comments:
Post a Comment