Kampuni ya Pennyroyal Gibraltar kupitia tawi lake la Best of
Zanzibar linalojihususha na shughuli za kusaidia jamii, imeanzisha masomo ya
usafi wa mazingira na afya kwa wanajamii wa maeneno ya Kijini and Mbuyu Tende
kaskazini mwa kisiwa cha Unguja.
Uhitaji wa elimu hii ulionekana baada ya kufanya utafiti
katika vijiji hivyo mwaka jana mwezi Desemba, na kuonekana kuwa kuna changamoto
kubwa sana za kiafya katika maeneo hayo ya Unguja Kaskazini. Utafiti ulifanyika
na maafisa afya sita kutoka Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA) wakisaidiana na
kampuni ya Pennyroyal ili kuweza kupata picha na hali halisi ya mahitaji ya
vijiji vya Kijini na Mbuyu Tende.
Baadhi ya matatizo yaliyogundulika
yalikuwa nipamoja na elimu finyu ya afya, usafi wamazingira na
ukosefu wa vyoo na maji safi.
Masomo haya yatafanyika katika awamu tano, yakianzia kwa
viongozi wa jamii wakiwemo masheha na wasaidizi wao, walimu na wanafunzi,
kwenye vikundi mbali mbali kama vya akina mama, wavuvi na vijana, na kwenye
mahospitali wakati wa kiliniki za kina mama.
Bi Nahya Nassor Khamis, afisa afya alisema ‘Changamoto
katika vijiji hivi vya Kijini na Mbuyu Tende niukosefu wa elimu ya afya na
usafi wa mazingira ambapo inachangia kwa
kiasi kikubwa kuleta matatizo kwa jamaii ikiwemo magonjwa ya milipuko kwamfano
kipindu pindu, maradhi ya ngozi na magonywa ya tumbo.’
Bi. Nahya akiwa na
maafisa wenzake na wafanyakazi wa Pennyroyal kwenye shule ya Kijini aliendelea
kusema, ‘Sasa chini ya usimamisi wa mradi wa Best of Zanzibar na kampuni ya
Pennyroyal tunauwezo wakuwasaidia wananchi wa Unguja Kaskazini kubadilisha
tabia zao na kujiepusha na maradhi yatokanayo na ukosefu wa elimu ya usafi.’
Bwana Mohamed Issa Khatib msimamizi wa mradi huo toka Best
of Zanzibar alisema, ‘Tulipo fanya utafiti mwaka jana tuligundua asilimia kubwa ya wananchi wa
Unguja Kaskazini wanachangamoto mbali mbali zaki maisha. Tumeanza na elimu ya
usafi, na kampuni yetu inajitolea kuendelea kuwapa fursa wanawake na vijana wa
jamii hizi kupitia masomo ya biashara ili waweze kujiendeleza kimaisha na
kupata ujuzi zaidi.
Tunaamini kwamba kupitia elimu hii ya biashara na ujuzi
wakutengeneza bidhaa mbalimbali kama vikapu na sabuni , na mafunzo ya kilimo wananchi
wa Kijini na Mbuyu Tende wanaweza kujikwamua kimaisha. Tunaamini kwamba bidhaa
hizi zitazotengenezwa na wanajamii hawa zitakuwa kiuvutio kikubwa kw watalii,
na wananchi wataweza kuziuza kwa watali hawa na kupitia Zanzibar Amber Resort
pale itakapo kamilika na ujenzi.’
Elimu hii itatolewa kwanzia tarehe 27 Februari na awamuya
kwanza itakamilika tarehe 9 Marchi 2017.
(Taarifa imetolewa na
meneja msimamizi wa Best of Zanzibar Tia Egglestone)
No comments:
Post a Comment