Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein walipokutana kwa mazungumzo Ikulu ya Chamwino mjini Dodoma leo Jumatatu Machi 13, 2017.
Picha na IKULU
STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Dodoma 3.3.2017
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein leo amefanya
mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Joseph
Magufuli katika Ikulu ya Chamwino
iliyoko mjini Dodoma.
Viongozi hao wawili
wamezungumzia mambo mbali mbali kuhusiana na masuala ya kimaendeleo pamoja na
kazi kubwa iliyoko mbele yao katika kuleta maendeleo na ustawi wa wananchi wa
pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aidha, Dk. Magufuli
ameitumia fursa hiyo kumpongeza Dk. Ali Mohamed Shein na kumtakia heri katika
siku yake muhimu ya kuzaliwa ambayo ni leo tarehe 13 Machi 2017. Dk. Shein alizaliwa
tarehe kama hiyo mwaka 1948 na hivyo kutimiza umri wa miaka 69.
Dk. Shein alisema kuwa ameitumia
siku yake hiyo ya kuzaliwa kwa kumtembelea Dk. Magufuli ili waweze
kubadilishana mawazo kwani wana kazi kubwa ya kujenga nchi pamoja na kuwaletea
maendeleo endelevu wananchi wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kutumia
fursa hiyo kumshukuru Dk. Magufuli kwa kumtakia heri katika siku yake hiyo
muhimu ya kuzaliwa.
“Siku ya kuzaliwa ni siku ya furaha lazima ikumbukwe, lazima
isherehekewe, mimi siku yangu ya kuzaliwa sisherehekei sana lakini huwa
nafurahi sana na leo nimefurahi sana” amesema Dk. Shein.
Dk. Shein ambaye pia, ni
Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, amerejea Zanzibar leo akitokea Mkoani Dodoma
ambako alishiriki vikao mbali mbali vya CCM, ikiwa ni pamoja na Mkutano Mkuu
Maalum wa CCM uliofanyika hapo jana.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment