Habari za Punde

RC Maseza Awaonya Wazazi Kuacha Kuwatuma Watoto Nyakati za Usiku na Kuwalaza na Wageni Chumba Kimoja

Mkurugenzi  wa asasi  isiyo ya  kiserikali ya  R.D.O ambayo  inajihusisha na  huduma  za  kijamii wilaya ya Mufindi na Kilolo Fidelis  Filipatali akimkabidhi mkuu  wa mkoa  wa  Iringa Amina Masenza zawadi ya  keki
Mkuu  wa  mkoa wa Iringa  Amina Masenza  akiwa katika  picha ya  pamoja na  watenda kazi wa R.D.O
Filipatali  akimkabidhi keki mkuu wa mkoa Masenza  kwa ajili ya katibu tawala wa Iringa
Wanawake  wakiwa na furaha  tele
Mkuu  wa mkoa  wa Iringa Amina Masenza  kulia na mwenyekiti wa UWT Mufindi  Marcelina Mkini  wakichota maji
Diwani  wa kata ya  Mdabulo akiwa amebebwa  juu juu na  wanawake baada ya  diwani huyo  kuimba shairi  lenye mvuto kwa  wanawake
Mkurugenzi wa R.D.O Bw  Filipatali  kulia  akiuongoza  msafara wa  mkuu   wa mkoa wa Iringa
Mkuu  wa mkoa wa  Iringa Amina Masenza  akiwahutubia  wanawake
Katibu  wa CCM wilaya ya  Mufindi Jimson Mhagama  kulia  na mwenyekiti wa UWT  Mufindi Marcelina Mkini  na mratibu wa  wanawake mkoa  wa Iringa mama  Sanga  wakifuatilia  hotuba ya  mkuu wa  mkoa
Watumishi  ofisi ya  RC  Iringa  wakitoa  zawadi kwa  ajili ya Yatima
Wasanii  wa Ibwanzi  wakiigiza  kama  Rais
Mkuu  wa  mkoa  akitembelea  banda ya  benki ya Mucoba
Mkuu wa  mkoa akipokea  risala ya  R.D.O
Kazi zinazofanywa na wanafunzi wa R.D.O
Mwenyekiti wa  sherehe  za  wanawake  Mufindi
Wafanyakazi ofisi ya  mkuu wa mkoa  wakiingia kwa maandamano 
Wanafunzi  wa sekondari ya  Mdabulo  wakicheza  igizo la unyanyasaji wa mwanamke
Mkuu  wa mkoa wa Iringa Amina Masenza  akitoa msaada kwa yatima  wanaolelewa na R.D.O
Wafanyakazi ofisi ya  mkuu wa mkoa  wa Iringa  wakitoa  misaada  yao kwa  yatima
Mkuu wa  mkoa wa  Iringa Amina Masenza na mwenyekiti  wa  UWT Marcelina Mkini ambae  ni  mjumbe wa NEC Taifa  kutoka  wilaya ya Mufindi  wakimtwisha  ndoo ya maji mmoja  kati ya  wanawake  wakazi wa Ikanga  kata ya Mdabulo  wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji  uliofadhiliwa na RDO























Mkuu  wa mkoa  wa Iringa  Amina  Masenza  akiwa na wa wafanyakazi wa RDO  na viongozi wa  wilaya ya Mufindi mara  baada ya  kumalizika kwa sherehe za  siku ya  wanawake  duniani
Mkuu  wa mkoa  wa Iringa  Amina Masenza kushoto na mwenyekiti wa UWT  Mufindi Marcelina Mkini  wakiongoza  maandamano ya  wananchi  Ikanga  kata ya  Mdabulo
Wanawake  kutoka  ofisi ya  mkuu wa mkoa  wa Iringa
Na  MatukiodaimaBlog
MKUU  wa mkoa wa Iringa Amina Masenza awataka wananchi mkoani hapa kutowaruhusu wageni kulala na watoto chumba kimoja. 








Kuwa kuanzia sasa mgeni akifika nyumbani kwako apewe godoro na kulala sebuleni na sio kushusha watoto vitandani na kumpa heshima mgeni Kulala kitandani chumba cha watoto.

Mkuu huyo wa mkoa ametoa ushauri huo leo wakati akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Ikanga kata ya Mdabulo wilayani Mufindi ambako maadhimisho  ya  siku ya  wanawake Duniani yalifanyika kwa mkoa wa Iringa. 

Alisema kuwa hatua kuwapa vitanda vya ama wageni kuchanganywa chumba kimoja na watoto baadhi yao si wema wapo kwa ajili ya kuwabaka watoto hao"


Pia aliwataka wazazi kutowatuma watoto nyakati za usiku madukani ama nje ya nyumba zao kwani kuendelea kuwatuma watoto hao usiku ni kuwahatarishia usalama wao na wabakaji 


Alitaka ikifika usiku wazazi wenyewe mama na baba ndio watumane dukani kama hakuna mtu mzima wa kutumwa na sio mtoto mdogo


Katika hatua nyingine mkuu huyo wa mkoa amepongeza taasisi isiyo ya Kiserikali ya RDO inayojishughulisha na huduma mbali mbali za kijamii wilayani Mufindi ikiwemo ya maji na malezi ya yatima. 


Pamoja na kuishukuru taasisi hiyo ya  RDO chini ya mkurugenzi wake Fidelis Filipatali, bado aliwaonya baadhi ya wanasiasa wanaotaka kukwamisha mradi wa maji kwa kuingiza siasa. 


Kuwa mradi huo wa maji hauna siasa na kuwa wananchi wanahitaji maji na sio siasa na kuahidi kuendelea kuwa karibu na asasi hiyo ya RDO. 

Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mufindi Marcelina Mkina ambae mjumbe wa NEC Taifa kutoka wilaya ya Mufindi na katibu wa CCM wilaya ya Mufindi walimpongeza Rais Dkt John Magufuli kwa kumteua Masenza kuwa mkuu wa mkoa wa Iringa na kuwa maendeleo na ushirikiano mkubwa wa serikali na chama umefanikisha maendeleo Kwa wananchi. 

Mkini alisema kuwa pongezi za utendaji kazi wa mkuu huyo wa mkoa atazifikisha rasmi kwenye mkutano mkuu wa CCM .

Hata hivyo alipongeza mapambano dhidi ya dawa za kulevya yanayofanya na serikali ya awamu ya tano pamoja na Vita dhidi ya ufisadi na rushwa na kuwa wao UWT na CCM wapo pamoja na Rais

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.