Habari za Punde

Nafazi za masomo Al Azhar University Misri

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR INATANGAZA NAFASI ZA MASOMO SHAHADA YA KWANZA NA YA PILI NCHINI MISRI KATIKA CHUO CHA “AL-AZHAR” KWA MWAKA WA MASOMO 2017/18.
SIFA ZA MUOMBAJI

SHAHADA YA PILI

· Awe Mzanzibari.
· Awe amemaliza Shahada ya kwanza
· Awe na afya nzuri
 · Awe hajajiunga na chuo chengine.

SHAHADA YA KWANZA

· Awe mzanzibari.
· Awe amemaliza kidato cha sita au Stashahada.
· Awe na afya nzuri.
· Awe hajajiunga na chuo chengine.

NJIA YA KUFANYA MAOMBI

Waombaji wote wanatakiwa kuwasilisha maombi yao Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, wakiambatanisha vitu vifuatavyo:-

· Kivuli cha kitambulisho cha Mzanzibari
· Vivuli vya vyeti vya masomo
· Kivuli cha cheti cha kuzaliwa.
· Kivuli cha pasi ya kusafiria
· Fomu ya uchunguzi wa afya.(medical report)

FANI ZINAZOTOLEWA Ni za Art na Science

NJIA YA KUTUMA MAOMBI

Maombi yote yatumwe kwa anuani ifuatayo:-

Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, S.L.P 394 Zanzibar.

IMPITIE

Mkuu wa Kitengo Cha uratibu Elimu ya Juu, Sayansi na Teknologia, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Zanzibar.
Lugha itakayotumika katika masomo hayo ni lugha ya Kiarabu

Kwa maelezo zaidi fika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mazizini chumba namba 57


MWISHO WA KUTUMA MAOMBI HAYO NI TAREHE 1/6/2017

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.