Habari za Punde

Waziri wa Afya Zanzibar afanya ziara ya kushtukiza Hospitali kuu ya Mnazimmoja

Na Mwandishi wetu

WAZIRI  wa Afya mhe. Mahmoud Thabit Kombo amefanya ziara ya kushtukiza katika hospitali kuu ya Mnazimmoja na kukuta kasoro mbali mbali za kiutendaji ikiwemo walinzi wanaolinda hospitalini hapo baadhi yao hawapo katika sehemu zao za kazi na walinzi  wengine wakiwatolea lugha zisizoridhisha baadhi ya watu waliofika hospitalini hapo.

Ziara hiyo alioifanya  usiku wa kuamkia leo ambapo aliweza kutembelea wodi vitengo mbali mbali na kuwakuta wafanyakazi wakiwa katika sehemu zao wakiwahudumia wagonjwa licha ya kuwepo kwa upungufu wa wafanyakazi baadhi  ya wodi.

Kutokana  hali hiyo ameuagiza Uongozi wa Hosptali hiyo kuchukua hatua stahiki katika kukabilina na matatizo mbali mbali yanayojitokeza ikiwemo suala la walinzi wanaolinda hospitalini hapo  kwa lengo la kuwapatia wananchi huduma bora za afya.

Alifahamisha ziara yake hiyo imeweza kubaini changamoto za wafanyakazi zikiwemo upungufu wa wafanyakazi ambapo ameahidi kulitafutia ufumbuzi suala hilo  haraka iwezekanavyo ili kuweza kufanikisha utendaji wa kazi katika hospitali hiyo ambayo ndio kimbilio la wananchi .

Katika ziara yake hiyo Mheshimiwa Mahamoud ameweza kutembelea sehemu mbali mbali ikiwemo wodi ya wazazi, sehemu ya upasuaji, kitengo cha huduma za dharura, wodi za wagonjwa Mahatuti, wodi zote za wanaume na wanawake pamoja na sehemu ya X ray na kuwakuta wafanyakazi wakiwa katika sehemu zao wakiendelea kuwahudumia wagonjwa.

Alifahamisha kuwa ziara hizo za kushtukiza katika Hospitali kuu ya Mnazimmoja  na hosptali nyengine zote za Unguja na Pemba  zitakuwa endelevu kwa lengo la kuwabaini wafanyakazi ambao watakiuka maadili ya kazi zao na kuwachukulia hatua ili kuepuka malalamiko kwa wananchi.


Ziara hiyo  ya Waziri wa Afya katika Hospitali kuu ya Mnazimmoja imekuja kufuatia hoja mbali mbali za wajumbe wa baraza la wawakilishi zilizoibuka katika baraza hilo na Waziri wa Afya kuahidi kuzifanyia kazi.

kuwa inatokana na ahadi yake Mhe. Waziri wa Afya ya kushuka chini Ngazi ya Utendaji ili kuhakikisha ufanisi, Uwajibikaji na Usimamizi na kuwataka Watendaji wote waungane nae mkono badala ya kulalamika kuwa wanaingiliwa katika majukumu Yao. 

Majukumu yote ya Wizara ya Afya na Hospitali pamoja na Vituo vyake vyote Vya Afya vipo chini ya Dhamana ya Wizara Ya Afya ambapo yeye Waziri wa Afya ndiye aliye na Dhamana Kuu ya Wizara hiyo katika Usimamizi na Utendaji ulio bora katika kutoa Huduma kwa Wananchi wote ww Zanzibar bila ya Ubaguzi wa Aina yoyote. 

Pia Mhe. Waziri wa Afya ametoa tamko la kushirikisha Kitengo cha Huduma kwa Jamii na Ustawi Wa Jamii kushirikishwa kikamilifu pale panapokuwa na tatizo ama upungufu wa Huduma au Mawasiliano kwa Wagonjwa na Wauguzi wanaotokana na Familia zao." .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.