Habari za Punde

Makamu wa Rais Mama Samia atembelea banda la Zantel Maonesho ya sabasaba

 Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Mama Samia Hassan Suluhu (wa pili kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mfanyakazi wa Kampuni ya Zantel alipotembelea banda la Kampuni hiyo katika maonyesho ya 41 ya Kimataifa ya Dar es salaam maarufu kama Sabasaba yanayoendelea hivi sasa katika viwanja vya Mwl J.K Nyerere. Kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na uwekezaji Mhe. Charles Mwijage na wa pili kushoto ni Meneja wa Data na Vifaa vya intaneti wa Zantel, Hamza Zuheri.
Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Mama Samia Hassan Suluhu akifurahia jambo na wafanyakazi wa Zantel alipotembelea banda la Kampuni hiyo katika maonyesho ya 41 
 Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Mama Samia Hassan Suluhu akimpongeza Mratibu wa Masoko wa Zantel-Zanzibar, Haji Khatib kwa kuchangia damu kwa hiari baada ya kiongozi huyo kutembelea banda la kampuni hiyo jana jijini Dar es salaam ili kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa. Zantel kwa kushirikiana na Mpango wa Taifa wa damu Salama wameandaa utaratibu wa uchangiaji damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya watu wenye uhitaji wa huduma hiyo katika kipindi hiki cha maonyesho ya 41 ya Kimataifa ya Dar es salaam maarufu kama Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwl J.K Nyerere. 
 Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Mama Samia Hassan Suluhu akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Data na Vifaa vya intaneti wa Zantel, Hamza Zuheri alipotembelea banda la Kampuni hiyo katika maonyesho ya 41 ya Kimataifa ya Dar es salaam maarufu kama Sabasaba yanayoendelea hivi sasa katika viwanja vya Mwl J.K Nyerere. 
 Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Mama Samia Hassan Suluhu akisalimiana na  Meneja wa Data na Vifaa vya intaneti wa Zantel, Hamza Zuheri (Katikati) alipotembelea banda la Kampuni hiyo katika maonyesho ya 41 ya Kimataifa ya Dar es salaam maarufu kama Sabasaba yanayoendelea hivi sasa katika viwanja vya Mwl J.K Nyerere. Kulia ni Meneja wa Chapa na Mawasiliano wa Zantel, Rukia Mtingwa.
Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Mama Samia Hassan Suluhu akisalimiana na  Meneja wa Chapa na Mawasiliano wa Zantel, Rukia Mtingwa alipotembelea banda la Kampuni hiyo katika maonyesho ya 41 ya Kimataifa ya Dar es salaam maarufu kama Sabasaba yanayoendelea hivi sasa katika viwanja vya Mwl J.K Nyerere. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.