Na.Haji Nassor - Pemba.
JAMII kisiwani Pemba, imetakiwa kuona
vibaya na aibu kutumia fedha zinazotokana na sulhu za kesi za watoto wao
waliobakwa au kulwitiwa, kwani kufanya hivyo hakusaidii kupunguza matendo hayo.
Akizungumza
na wananchi wa shehia za Ukutini Jimbo la Chambani wilaya ya Mkoani na shehia
ya Wingwi mapofu wilaya ya Micheweni
Pemba, Afisa Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba,
Khalfan Amour Mohamed, alipokuwa akizungumza na wananchi hao kwenye mikutano ya
kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi.
Alisema wapo
baadhi ya wazazi na walezi wamekuwa na mtindo wa kuzimaliza kienyeji kesi hizo
kwa kuchukua fedha ambazo kisha huzitumia kwa mahitaji ya kila siku.
Afisa
Mipango huyo alisema lazima jami ifike pahala ione aibu na fedheha kwa kukubali
kesi za watoto wao waliobakw au kulawitiwa kuchukua fedha ili zimalizike
kienyeji wakidhani kufanya hivyo ndio suluhu.
Alieleza
kuwa, wazazi hao wamekuwa wakifanya hivyo ikiwa ni aina moja ya rushwa ya
muhali, huku watoto wao wakikosa haki zao, na wafanyaji wa matendo hayo
kuendelea.
“Mbakaji au
mtu mwenye tabia ya kulawiti, akiona mzazi anapokea fedha baada ya tukio, basi
baada ya muda anafanya tena tendo hilo, lazima sasa mubadilike na muache
kuchukua fedha kama suluhu ya udhalilishaji huo”,alifafanua.
Kwa upande
wake Afisa Mipango wa Kituo hicho Siti Habibu Mohamed, aliwataka wananchi hao
kujenga utamaduni wa kuandikia kila wanapofanya mauziano.
Alisema wapo
baadhi ya wananchi wamekuwa wakinunua maeneo ya ardhi, nyumba, vyombo vya
usafiri bila ya kuwepo maandikiano jambo ambalo baade huzaa migogoro.
Sheha wa
shehia ya Wingwi mapofu Ali Hamad Saleh, alisema nafasi waliopewa wananchi wake
ni muhimu, maana wapo wanaohitaji msaada wa kisheri wakalazimika kutumia fedha
nyingi.
Aidha
alisema wakati umefika sasa kwa wananchi kuhakikisha wanajisomea sheria mbali
mbali, kwa kuwatumia wasaidizi wa sheria waliopo majimboni ili kufahamu haki na
wajibu wao.
Baadhi ya
wananchi wa shehia hizo wamekipongeza Kituo hicho kwa kuwafuata na kuwapa
msaada wa kisheria bila ya malipo, jambo ambalo limewapa mwanga wa kujua haki
zao.
Salama
Othaman Ramadhan mkaazi wa shehia ya Ukutini Jimbo kla Chambani alisema, sasa
ameelewa njia za kufanya iwapo mwanawe atabakwa, jambo ambalo kabla hakuwa na
taaluma.
“Mimi
ilikuwa najua kuwa mwanangu akishabakwa, kama watakubali tumaliziane kwa
suluhu, ilikuwa ndio dawa, lakini sasa kumbe hiyo ni kesi ya jinai, inatakiwa
ifikishwe mahakamani”,alifafanua.
Nae Asia
Saleh Salim alisema, ameshapata uwelewa juu ya njia za kufanya kisheria,
anapotaka kununua mali, ikiwa ni pamoja na kuifanyia uhakiki iwapo haina
migogoro.
Kwa upande
wake mwananchi wa shehia ya Wingwi mapofu wilaya ya Micheweni, Ali Juma Hamad alisema
jamii lazima iongezewe dozi ya elimu juu ya athari za kuzifanyia sulhu kesi
hizo.
Nae Kombo
Juma, amesema sasa anaelewa kuwa kumbe Halmashauri inayo mamlaka ya kumpandisha
mtu kwenye mahakama zake, iwapo watakwenda kinyume na maagizo.
“Elimu ya
ufafanuzi wa masuali yetu imenipa uwelewa na sasa kilichobakia nyinyi Kituo cha
Huduma za Sheria endeleeni kutupia vijijini kwetu ili tujue haki na wajibu wetu
kisheria”,alifafanu.
Akitoa
ufafanuzi haki za mtoto Afisa Mipango wa Kituo hicho Mohamed Hassan Ali,
alisema wakati umefika kwa jamii kuwa na malezi ya pamoa ili kukomesha mtendo
maovu yanayofanywa na watoto.
“Njia
mwafaka ambayo inaweza kuwatoa watoto wetu kwenye majanga yaliopo ni
kuhakikisha tunasaidiana kimalezi badala ya utaratibu wa sasa wa kila mmoja
kulea mwanawe”,alifafanua.
Kituo cha
Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, tayari kimeshwatembelea waanchi
wa shehia za Mbuyuni, Ukutini, Winwgwi mapofu, Wesha, Kiwani, Kengeja,
Shengejuu, Kinowe. Mgogoni, na Kiungoni kuwapa msaada wa kisheri bila ya
malipo.
No comments:
Post a Comment