Na.Haji Nassor - Pemba.
WANAWAKE wa shehia ya Vitongoji
wilaya ya Chakechake kisiwani Pemba, wamesema kujiunga kwao kwenye vikundi vya
kuweka na kukopa, ‘hisa’ ni hatua muhimu kwao kuwasaidia waume zao huduma za
kila siku, hasa kwa vile hutokezea siku wanakosa.
Walisema
wanaume hawana mkataba na Muumba, kwamba kila siku watakuwa wanakamilisha hudua
za ndani ya nyumba, hivyo kuingia kwao kwenye vikundi hivyo vya kuweka hisa,
pamoja na mambo mengine, lakini pia ni kuwasaidia wenza wao huduma za lazima.
Wakizungumza
na waandishi wa habari wa habari vyombo mbali mbali, wanawake hao walisema,
wamegundua iwapo mwanamme ndani ya nyumba atapewa msaada kwa baadhi ya siku,
hata ndoa zao hupata heshima na nidhamu.
Mwenyekiti
wa kikundi cha kuweka na kukopa cha ‘wema hauozi’ Maryam Saleh Juma, alisema ni
ukweli usiofichika yeye kabla ya kujiingiza kwenye vikundi hivyo, hakuona sana
thamani ya ndoa yake.
Alisema
wanaume wanaokuwa na wanawake wanaosubiri kila huduma kuletewa, hukosa furaha
ya ndoa zao, jambo linalohatarisha usalama na uendelevu wa ndoa husika, ingawa
iwapo mwanamke anamchango huwa tofauti.
“Mfano kama
mimi sasa nahisi mume wangu ananielewa kwenye ndoa, na amekuwa akinishirikisha
na kunishauri mambo ambayo kabla nikiona anafanya uamuzi tu peke yake”,alifafanua.
Nae Katibu
wa kikundi hicho Zena Khamis Juma, alisema yeye kupitia uwanaharakati wake wa
upandaji wa mboga mboga na kujiwekea akiba, sasa amefanikiwa kujenga nyumba ya
pili kwa kushirikiana na mume wake.
Alieleza
kuwa, ingawa kiwango kikubwa cha fedha alizokuwa akiziweka kwenye hisa akipewa
na mume wake, lakini tayari nyumba hiyo imekamilika na sasa mume wake ameongeza
mke wa pili.
“Mimi
sijaona vibaya mume wangu kuongeza mke kwa kushirikiana nguvu zake na zangu,
maana nilimruhusu na sasa nimepata nguvu zaidi ya kuendelea na ujasiriamali na
yeye amenikubali”,alifafanua.
Alisema kwa
sasa, wameshakamilisha ujenzi wa nyumba ya kisasa yenye thamani ya zaidi ya
shilingi milioni 30, na hana wasiwasi wa kuwahudumia watoto wake kwa vifaa vya
madrassa na skuli.
Nae mume wa
mjasiriamali huyo Juma Abrahaman Said, alikiri kuokolewa kimaisha na mke wake
huyo kutokana na ujasiriamali wake anaoendelea nao.
Alifafanua
kuwa msaada mkubwa anaoupata kwa mke wake huyo umemuwezesha kujenge nyumba ya
pilia, ambayo anasema asilimia 40 ya gharama pamoja na nguvu kazi zilitokana na
mke wake.
“Mimi hata
nikiamua nyumba kutaka kuiza na tukikubaliana kuiuza kwa shilingi milioni 30,
basi twazigawa sawa sawa, maana kama sio yeye mimi nisingepaya ujasiri wa
kujenga nyumba”,alifafanua.
Hata hivyo
amewakumbusha wanaume kuacha dhana potofu kuwa wanawake wanapojiingiza kwenye
ujasiriamali ni uhuni na usema huko ndio wanakofikia ndoto zao.
Nae
Mwenyekiti wa kikundi cha Tumain kinachojishughulisha na ukulima wa mboga mboga
Mtuwa Ali Vue, alieleza kuwa lazima wanaume waache mzaha wa kuwafungia wake zao,
na badala yake wawape uhuru wa kujiletea maendeleo.
“Wakati
umefika sasa kwa wanawake kujiwezesha, kinachotakiwa ni kwa wanaume waliomo kwenye
ndoa kuhakikisha, wanawaruhusu wake zao maana wakiwafungia watawazidisha
umaskini”,alifafanua.
Hata hivyo Shamim
Haji Makame, alisema bado wapo baadhi ya wanaume hawajaona umuhimu wa wanawake
kuwa na chao, jambo linalopelekea ugumu, kwa baadhi ya wanawake kuijiingiza
kwenye vikundi vya ujasiriamali.
Mkubwa Ali
Mkubwa ambae ni mjasiriamali aliewaajiri wanawake watatu kwenye shamba lake la
mboga mboga alisema, kama bado kuna wanaume wamekuwa wazito kuwaruhusu wake zao
kuijiingiza kwenye umoja wa kujiletea maendeleo, wamechelewa kuamka.
“Hivi sasa
tofauti ya mwanamke na mwanamme ni ile ya kimaumbile tu, lakini kwenye kusaka
toke, watu wote wako sawa, maana maisha ya kuwa goli kipa hasa kwenye ndao yamekwisha”,alifafanua.
Omar Mjawiri
Hamad yeye anasema, bado hajaamua mke wake kumpeleka shambani, kushughulikia
kilimo kwa vile yeye mwenyewe anamudu kazi hiyo.
Sheha wa
shehi ya Vitongoji Salum Ayoub Suleiman alisema, kwenye shehia yake, baada ya
wanawake kupata elimu ya ujasiriamali, sasa hali za maisha yao hasa kwa waliomo
ndani ya ndoa yamebadilika.
“Sasa
mwanamke wa Vitongoji akiwa anahitaji fedha kwa ajili ya harusi, fedha za vifaa
vya skuli, msiba au michango mengine ya familia, basi hukopa kwenye hisa au
huuza mboga mboga”,alifafanua.
Hata hivyo
wakulima hao wa mboga mboga shehiani humo, wamesema kwa sasa changamoto kubwa
inayowarejesha nyuma ni ukosefu wa soko la uhakika.
Shehia ya
Vitongoji wilaya ya Chakechake pekee, inajumla vikundi vya mboga mboga 15 na
vya ufugaji 20, hisa 45 na vya ufugaji wa nyuki zaidi ya 10.
No comments:
Post a Comment