Habari za Punde

Mchezo wa Ufunguzi wa Michuano ya UBA Basket Ball Zanzibar Kati ya Mbuyuni na Polisi Uliofanyika Uwanja wa Maisara Mbuyuni Imeshinda kwa Vikapu 50-48.

Mchezaji wa Timu ya Polisi Zanzibar akijaribu kumpita mchezaji wa Timu ya Mbuyuni wakati wa mchezo wao wa Ufunguzi wa Michuano ya UBA inayofanyika katika viwanja vya Maisara Zanzibar Timu ya Mbuyuni imeshinda kwa vikapu 50-48. Michuano hiyo imedhaminiwa na Wamarekani. 



Mchezaji wa Timu ya Mbuyuni akijiandaa kufunga katika mchezo huo.
Hekaheka katika goli la timu ya Polisi wakati wa mchezo huo wa ufunguzi uliofanyika uwanja wa maisara Zanzibar Timu ya Muyuni imeshinda kwa vikapu 50-48.
Wachezaji wa Timu ya Mbuyuni wakishangilia kikapu cha ushindi dhidi ya Timu ya Polisi wakati wa mchezo wao wa ufunguzi wa michuano ya Kombe la UBA inayofanyika viwaja vya maisara Zanzibar ikiwa chini ua udhamini wa Marekani. 
Wapenzi wa Timu ya Mbuyuni wakiishangilia Timu yao wakati wa mchezo wao wa ufunguzi wa Michuano ya UBA Basket Ball inayofanyika katika viwanja vya maisara Zanzibar.
Wachezaji wa Timu ya Mbuyuni na wapenzi wao wakishangilia ushindi wao wa mchezo wa ufunguzi dhidi ya Timu ya Polisi baada ya kuibuka na ushindi wa Vikapu 50-48.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.