Habari za Punde

Ligi kuu kanda ya Pemba yarudi dimbani leo Okt, 23.

Na.Haji Nassor - Pemba.
LIGI kuu ya Zanzibar kanda ya Pemba, inatarajiwa kuendelea tena leo, kwenye viwanja viwili tofauti, ambapo kwenye uwanja wa FFU Finya, Okapi yenye point nne, wakiwaalika Opec yenye point mbili.

Katika uwanja wa Gombani, wenyeji wa uwanja huo, timu ya Younger Islanders yenye pointi sita, ikishika nafasi ya pili, itawakarabisha Hard rock ambayo ina point mbili, tayari timu zote zimeshashuka uwanjani mara tatu.

Kesho ni zamu ya wakongwe wa soka wa Jamhuri, yenye point  nne, ikishika nafasi ya tatu, watakaoumana na Chuo basra yenye point mbili, mchezo unaotarajiwa kuchezwa uwanja wa FFU Finya majira ya saa 10:00 jioni.

Kesho hiyo pia, ndani ya dimba la Gombani New star yenye point nne, itawakuwa wageni wa FSC yenye pointi sita, baada ya kushinda michezo miwili na kufungwa mmoja.

Wakati ligi kuu ya Zanzibar kituo cha Pemba, ikitoka kwenye mapunziko mafupi, baada ya kuendelea tena leo, timu ya Mwenge ndio vinara wa ligi hiyo, ikijikusanyia point tisa, wakati Islanders, FSC na Shaba wakikabana koo kwenye nafasi ya pili kwa point sita.


Timu zinazoshindana kukokota mkia wa ligi kuu Zanzibar kituo cha Pemba, ni pamoja na Wawi star yenye point moja, Opec, Dodo moro, Chuo basra na Hard rock zikivutana kwa kuwa na pointi mbili mbili, baada ya kucheza michezo mitatu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.