Habari za Punde

Makamu wa Rais afungua kongamano la kimataifa la Utalii

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa kufungua Maonyesho ya Tatu ya Kimataifa ya Utalii yanayojulikana kwa jina la Swahili linalofanyika kwenye kituo cha mikutano cha kimataifa cha Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamis Kigwangalla akihutubia wakati wa Ufunguzi wa Maonyesho ya ya Tatu ya Kimataifa ya Utalii ya Swahili uliofanyika kwenye kituo cha mikutano cha kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi kinyago maalum Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANAPA Jenerali Mstaafu George Waitara kama ishara ya shukrani kwa kuwa mmoja wa wadhamini wa Maonyesho ya Tatu ya Utalii ya Kimataifa ya Utalii ya Swahili.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Bw. Allan Kijazi mara baada ya kupokea kinyago maalum ikiwa ni shukrani kwa kuwa mmoja wa wadhamini wa Maonyesho ya Tatu ya Utalii ya Kimataifa ya Utalii ya Swahili. 
   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi kinyago maalum Naibu Mhifadhi (Uhifadhi, Maendeleo ja Jamii na Utalii) wa Hifadhi ya Ngorongoro Dkt. Maurus Msuha kama ishara ya shukrani kwa kuwa mmoja wa wadhamini wa Maonyesho ya Tatu ya Utalii ya Kimataifa ya Utalii ya Swahili. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)




Picha ya Pamoja 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.