NA HAJI NASSOR,
PEMBA
MFUKO wa Maendeleo ya Elimu kwa Wanahabari Zanzibar
‘MMEWAZA ‘wenye makao makuu yake kisiwani Pemba, umeanza kutoa fedha za masomo
kwa wanachama wake, baada ya kukusanya fedha hizo kwa kipindi cha miezi mitatu
iliopita.
Kwa hatua za awali wanachama watano wanaosoma
kwenye vyuo mbali mbali, ambao waliwasilisha majina yao kwa uongozi wa Mfuko,
ndio waliopatiwa fedha hizo kwa ajili ya kuongeza fedha za masomo.
Akizungumza
kabla ya ugawaji wa fedha hizo, mweka hazina wa Mfuko huo Raya Ahmada, alisema
kutokana na makusanyo kutofikia lengo walilokusudia, walilazimika kuweka
kiwango cha shilingi 400,000 kwa kila mwanachama.
Alisema
awali, walitarajia kufikia wanachama 50, ili wakusanye shilingi 1500,000
(milioni moja na laki tano) kwa mwezi, ambapo miezi mitatu baadae, wajikusanyie
shilingi milioni 4. 5 ili kuwapatia shilingi milioni moja kwa wanachama wanne
kila miezi mitatu, ingawa mipango yao ilikuwa tofauti.
Mwekahazina
huyo, alisema kutokana na kukosa idadi kubwa ya wanachama kwa hatua za awali,
ndio maana wakalazimika kukusanya shilingi 690,000 kila mwezi kwa idadi ya
wanachama 23, kwa wastani wa shilingi 30,000 kwa mwanachama mmoja.
Hivyo
alisema wametumia shilingi milioni 2, kwa kuwakabidhi wanachama watano shilingi
400,000 kila mmoja, ili kuendelea mbele na masomo.
“Leo
(jana) tumeshawakabidhi wanachama wetu watano wa ‘MMEWAZA’ shilingi 400,000
kila mmoja, ambao hawa kwanza wako masomoni, na ndio walioleta majini yao
mwanzo”,alifafanua.
Hata
hivyo Mwekahazina huyo, alisema haina maana kuwa mwanachama ambae hasomi kuwa,
hatofaidika na mchango, bali kwanza ni kuwapatia wale walioko vyuoni ili wapate
utulivu wa masomo.
Katika
hatua nyengine, Mwekahazina huyo wa ‘MMEWAZA’ aliwataka wale waliopatiwa fedha
hizo, kuzitumia kwa lengo lililokusudiwa, ili kutimiza ndoto zao za kujisomea,
pamoja na malengo ya Mfuko kama ulivyoanzishwa.
Mapema
Katibu wa Mfuko huo Salmin Juma, alipongeza hatua ya ustahamilivu kwa wanachama
hao, hadi kufikia kupatiwa fedha hizo kwa ajili ya kujisaidilia kimasomo.
Alisema,
ipo mifuko kadhaa huanzishwa kwa lengo kama hilo, ingawa huwa hayafikii
kugawana kutokana na kujitokeza kwa mambo tofauti, ingawa kwa ‘MMEWAZA kwa
hatua za awali, umeanza vizuri.
“Ni
jambo la faraja kuona mfuko umeanza kugawa mapato kwa wanachama husika, maana
ipo mengi ambayo huanzishwa na kisha kuhesabu migogoro”,alifafanua.
Baadhi
ya wanachama waliokabidhiwa fedha hizo na kutopenda majaina yao yatajwe,
walisema wamefarajika kuona viongozi wamefikia malengo hayo.
Walisema,
ni wakati mwafaka kwa ambao hawajiunga kuhakikisha ukimalizika mzunguruko wa
kwanza, kujiunga ili wawe na uhakika wa kujipatia fedha zao, hasa kwa wale
wanaosoma.
Mfuko
wa Maendeleo na Elimu kwa Wanahabari Zanzibar ‘MMEWAZA’ ambao umeanzishwa mwezi
Juni, mwaka huu unawanchama 23, ambao kila mwezi hukusanya shilingi laki 690,000
na lengo kuu, ni kuwasaidia fedha za ada wanachama wao ambao wengi ni waandishi
wa habari.
No comments:
Post a Comment