Habari za Punde

Mwanamitindo Asya Idarous Khamis Kufunika Sherehe za Uhuru Oakland!

Tukiwa tunaelekea ukingoni mwa mwaka 2017 Mama wa mitindo maarufu hapa Tanzania kama Asya Idarous Khamsin, ambaye kwa sasa makazi yake ni nchini Marekani.  Ifikapo December 9th 2017  ataiwakilisha Tanzania kwa kuonyesha mitindo yake kwenye sherehe za uhuru Oakland Carlifonia.

Hivyo tukiwa kama Watanzania ni jambo la kujivunia maana Tasnia ya mitindo imekuwa ni moja kati ya vyanzo vizuri vya kuitangaza nchi yetu. Tunapaswa kuonyesha ushirikiano kwa wabunifu (Designers)  wetu wanao jituma kama Mama yetu Asya Idarous Khamsin na wengineo.

Ukiguswa unaombwa kusambaza ujumbe huu kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki wanao penda Fashion  Asante.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.