Manahodha wa Timu za Libya na Tanzania bara wakiwa katika picha ya Pamoja kabla ya kuanza mchezo wao . Mechi ilimalizika kwa sare ya bila kufungana
Kikosi cha Timu ya Libya ambacho kinashiriki mashindano ya CECAFA kama mwalika kklichomenyana na Timu ya Taifa ya Tanzania Bara , Kilimanjaro Stars
Na Abubakar Khatib Kisandu, Machakos Kenya.
Wenyeji wa Mashindano ya CECAFA SENIOR CHALLENGE CUP timu ya Taifa ya Kenya wameenza vyema baada ya leo kuifunga Rwanda mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa saa 8 za mchana katika uwanja wa Bukhungu huko Kakamega .
Mabao ya Kenya yamefungwa na Maasud Juma na Dancon Otieno.
Na katika uwanja wa Kenyata huko Mjini Machakos timu ya Taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) wakatoka sare ya 0-0 dhidi ya Libya.
Mashindano hayo yataendelea tena kesho kwa kupigwa mchezo mmoja kati ya Uganda dhidi ya Burundi Saa 9:00 Alaasiri katika uwanja wa Bukhungu huko Kakamega .
No comments:
Post a Comment