SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
WIZARA YA HABARI UTALII UTAMADUNI NA MICHEZO
Tel: 0255 24 2237325/0255 24 223 7313 Idara ya Habari Maelezo
Fax: 0255 24 2237314
P.O.
Box 2754
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
(TANZIA)
Kesho saa 6:00 mchana mwili wa askari wa Jeshi la
Wananchi wa Tanzania Marehemu SGT Issa Saleh Issa aliyekuwa majeruhi akipatiwa
matibabu nchini Uganda baada ya shambulio la Waaasi Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Congo utawasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume
Terminal I.
Marehemu SGT Issa Saleh Issa alikuwa katika Kikosi cha
Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa nchini DRC.
Baada ya kuwasili kwa maiti hiyo, itapelekwa moja kwa
moja Kijijini kwao Ndijani Wilaya ya Kati Mkoa Kusini Unguja kwa mazishi.
Imetolewa na :-
Dk. Juma Mohammed Salum
KNY
Mkurugenzi
Idara ya Habari (MAELEZO) Zanzibar
Zanzibar
29, Desemba, 2017.
No comments:
Post a Comment