Mwenyekiti wa Kamati iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuchunguza biashara ya madini ya Tanzanite ambaye ni Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akisalimiana jijini Dar es salaam leo Januari 17, 2018 na wawakilishi wa kampuni ya Tanzanite One kabla ya kuanza na mazungumzo ambayo yanalenga kuhakikisha Tanzania inanufaika ipasavyo na rasilimali ya madini hayo ambayo yanachimbwa nchini Tanzania pekee. Picha na IKULU
JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI
YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
Simu: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Faksi: 255-22-2113425
|
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Kamati
iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe
Magufuli kuchunguza biashara ya madini ya Tanzanite imeanza kufanya mazungumzo
na kampuni ya Tanzanite One.
Mwenyekiti
wa kamati hiyo ambaye ni Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi
amesema mazungumzo hayo yaliyoanza tarehe 16 Januari, 2018 yanalenga
kuhakikisha Tanzania inanufaika ipasavyo na rasilimali ya madini hayo ambayo yanachimbwa
nchini Tanzania pekee.
Prof.
Kabudi amesema mazungumzo yameanza vizuri ambapo pande hizo mbili zinapitia
matatizo yote yanayohusu biashara ya madini ya Tanzanite, utekelezaji wa sheria
na kanuni mbalimbali za madini na mapato ya rasilimali hiyo, ili hatimaye
zikubaliane namna bora itakayohakikisha Tanzania inanufaika ipasavyo.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Tanzanite One Bw. Faisal Juma Shahbhai amesema
Tanzanite One ipo tayari kwa majadiliano hayo na inaunga mkono juhudi za
kuhakikisha madini hayo yanainufaisha Tanzania tofauti na ilivyo sasa ambapo
yanazinufaisha zaidi nchi nyingine ambazo hazizalishi Tanzanite.
Bw.
Shahbhai ameongeza kuwa Tanzanite One itatoa taarifa zote zinazohitajika na
wakati wote itatoa ushirikiano wenye lengo la kufanikisha mazungumzo hayo.
Gerson
Msigwa
Mkurugenzi
wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar
es Salaam
17
Januari, 2018
No comments:
Post a Comment