Habari za Punde

Jumuiya ya Istiqaama yakabidhi misahafu kwa skuli zilizomo jimbo la Chwaka

Fatma Makame - Maelezo  Zanzibar 
Jumuiya ya Istiqaama Zanzibar ikishirikiana na Radio Adhana imekabidhi Misahafu 1,200 kwa Wanafunzi wa Skuli nne za Jimbo la chwaka Wilaya ya kati mkoa wa Kusini Unguja ikiwemo SKuli ya Chwaka,Marumbi, Pongwe na Koani.
Msaada wa Misahafu hiyo una lengo la kuwapatia Wanafunzi hao fursa ya kujifunza zaidi Dini ya kiislamu kupitia Misahafu hiyo.
Akizungumza na wandishi wa habari mara baada ya kukabidhi Misahafu hiyo Mwenyekiti huduma kwa jamii Jumuiya ya istiqaka Zanzibar Said Hamed Haroub amesema  lengo la kuwapatia Misahafu hiyo ni kuisoma na kuwa mwongozo wa maisha yao ya Dunia na akhera.
Amesema si vyema Misahafu hiyo kupuuzwa kwa kuifungia ndani badala yake wanatakiwa kuipa umuhimu katika maisha yao ya kila siku.
Amesema Wanafunzi hao wanapswa wakipe umuhimu Mkubwa kitabu hicho kitukufu kwa vile wanapokisoma kitachochea ufahamu mkubwa kwa masomo yao ya kawaida.
Aidha Mwenyekiti huyo amewataka wanafunzi wa skuli ya chwaka  kuitumia vizuri misahafu hiyo na kuyafata yale yaliyo amrishwa ndani ya kitabu hicho   na kutoyafanya yasiyo ya maana katika uislamu kwa kukabidhi misahafu   elfu moja miambili 1200 .
Kwa upande wake nae  Naibu Mkurugenzi  wa Radio Adhana Said Suleiman  amewataka wanafunzi hao kuisoma kur-ani kwa ajili ya kuchuma thawabu na  kujijengea maisha yenye kufuata mwongozo sahihi ya dini ya kislamu .
Nae Mwalimu mkuu wa skuli ya chwaka Tatu Shaabani Mayala  ametowa shukrani  kwa Jumuiya ya istikama kwa kuwapatia misahafu ambayo itakuwa kichocheo ya kuimarisha maadili mema ya Wanafunzi hao.
Amewahimiza Wanafunzi hao kukisoma Kitabu hicho na kurudi Chuoni kwa wanafunzi ambao wametoroka Vyuoni ili kuifahamu vyema dini yao.
Awali Diwani wa wadi ya Chwaka  Mlenge Khatibu Mlenge  ameipongeza jumuiya hiyo misaada hiyo ya kitabu cha Qur –ani na kuwataka wanafuzi kukitunza na kuvisoma  vizur  kwani ndicho chimbuko la elimu.

Imtolewa na Maelezo Zanzibar

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.