Habari za Punde

MEI MOSI KITAIFA IRINGA ,RAIS JPM KWA MARA YA KWANZA KUTUA IRINGA

 Rais  wa  shirikisho  la  vyama huru    vya  wafanyakazi Tanzania  (TUCTA) Tumaini  Vyamhokya katikati akiongoza  kuimba  wimbo wa  wafanyakazi  wakati wa  kikao  na  waandishi wa habari mkoa  wa  Iringa kuelezea maandalizi ya  Mei  Mosi  kitaifa  yatakayofanyika  mkoani Iringa
Mkuu  wa  wilaya ya  Iringa  Richard Kasesela kulia  akiwapongeza  viongozi wa  shirikisho  la  vyama  vya  wafanyakazi
Wajumbe  wa TUCTA  wakiimba  wimbo  wa  wafanyakazi  leo
Wimbo   wa  kuwaunganisha  wafanyakazi
Rais  wa  shirikisho  la  vyama huru    vya  wafanyakazi Tanzania  (TUCTA) Tumaini  Vyamhokya kulia  akiwa na  wajumbe  wenzake  .


Na. MatukiodaimaBlog.

SHIRIKISHO   la  vyama huru    vya  wafanyakazi Tanzania  (TUCTA) ambao  ni  waandaaji  wa  sherehe  za  wafanyakazi kitaifa  (MEI  MOSI) wamempongeza  Rais  Dkt  John Magufuli kwa  kukubali  mwaliko  wao  wa  kuwa  mgeni  rasmi katika sherehe  hizo za  Mei  Mosi  zitakazofanyika  kitaifa  mkoani Iringa .

Rais wa shirikisho  la  vyama huru    vya  wafanyakazi Tanzania  (TUCTA)  Tumaini  Vyamhokya alisema  leo  kuwa  katika  sherehe  hizo  za  wafanyakazi duniani kwa  Tanzania  zitafanyika  katika  mkoa  wa  Iringa kwenye  uwanja  wa  Samora  na  kuwa tayari  Rais Dkt  Magufuli  amekubali  kuwa  mgeni  rasmi .

 Hivyo  aliwataka  wafanyakazi   kujitokeza  kwa  wingi  kushiriki sherehe  hizo  na  kuwa  kupitia sherehe  hizo  watapata fursa ya  kujua  mikakati ya  serikali  dhidi ya wafanyakazi  nchini japo  hadi  sasa  wanapongeza  hatua  iliyofikiwa na  serikali ya  kuwarejesha  kazini  wafanyakazi  waliokuwa  wamesimamishwa kazi  kutokana na elimu  yao ya  darasa la  saba.

Rais   huyo  alisema  kuwa  TUCTA  imefanya  jitihada  kubwa  za  kukutana na  serikali  kuwapigania  wafanyakazi hao  walioondolewa kazini   kutokana na  elimu   yao na  serikali  imesikiliza  na  imewarejesha  kazini .

Alisema  kuwa  serikali  imeendelea  kufanya  jitihada  kubwa  kuongeza ajira  pamoja na  kusikiliza  kero  mbali mbali  za  wafanyakazi na  kuzipatia  majibu .

Akielezea  juu ya maandalizi ya  sherehe  za mei  mosi  mkoani  Iringa  alisema  kwa  sehemu  kubwa   maandalizi yanakwenda  vizuri na  wamepata  ratibu ya  kuzunguka  wilaya  zote za  mkoa  wa Iringa kutoa elimu  pamoja na kututana na  wafanyakazi ili  kujua  changamoto  zao.

 " TUCTA  inapenda  kuishukuru  serikali  ya  mkoa  wa Iringa kwa  kukubali  kupokea maadhimisho  haya  ya  Mei mosi 2018 TUCTA kwa  kushirikiana  na  serikali ya  mkoa wa  Iringa chini ya  mkuu wa  mkoa Amina Masenza pamoja na waziri  wa  nchi ofisi ya  waziri  mkuu  sera ,bunge  ,kazi ,vijana , ajira   na  watu  wenye  ulemavu Jenista Mhagama tumefanya maandalizi ya  kutosha"


Alisema  kabla ya  Mei  mosi  mambo  yakayofanyika  Iringa ni  pamoja na makongamano mawili ya  kimkoa na  moja la kitaifa  na kuwakongamano la kwanza  litafanyika April 23 katika  wilaya ya  Mufindi ambapo mgeni rasmi  atakuwa mkuu wa  wilaya ya Mufindi  Jamhuri  Wiliam wakati  kongamano la  pili  litafanyika  wilaya ya  Kilolo  April 25  na  mgeni  rasmi  ni mkuu wa  wilaya ya  Kilolo Asia Abdalah  huku April 27 litafanyika  kongamano la  kitaifa litakalohusu Tanzania ya  uchumi wa  viwanda kwenye  ukumbi wa  Kichangani ambalo  viongozi mbali mbali  wa  kitaifa  watashiriki .

Aidha  alisema  kutakuwa na  michezo  ya  Mei  mosi ya fani mbali mbali itakayoanza April 16 hadi  April 30 katika uwanja wa  Samora kuwa  kwa  ajili ya  kuwafanya  wafanyabiashara na  wajasilia mali  kutumia  fursa ya  mei  mosi  Iringa maonyesho  ya  bidhaa mbali  mbali yatafanyika .

 







No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.