Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa Kampuni ya "KUSHAN ASIA AROMA COOPERATION LIMITED" kutoka China Bw.Zhou Junxue akiwa na Ujumbe wa Viongozi aliofuatana nao leo walipofika Ikulu Mjini Zanzibar.[Picha na Ikulu] 09/04/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akimsikiliza Mwenyekiti wa Kampuni ya "KUSHAN ASIA AROMA COOPERATION LIMITED" kutoka China Bw.Zhou Junxue (katikati) walipokuwa katika mazungumzo na Ujumbe wa Kampuni hiyo walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo.[Picha na Ikulu] 09/04/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akimsikiliza Mwenyekiti wa Kampuni ya "KUSHAN ASIA AROMA COOPERATION LIMITED" kutoka China Bw. Zhou Junxue (kushoto) walipokuwa katika mazungumzo na Ujumbe wa Kampuni hiyo walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo (katikati) Bw.Guang William-Meneja Mauzo,[Picha na Ikulu] 09/04/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Mwenyekiti wa Kampuni ya "KUSHAN ASIA AROMA COOPERATION LIMITED" kutoka China Bw.Zhou Junxue (kushoto) walipokuwa katika mazungumzo na Ujumbe wa Kampuni hiyo walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo (katikati) Bw.Guang William-Meneja Mauzo,[Picha na Ikulu] 09/04/2018.
STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 09.04.2018
RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameipongeza Kampuni ya
‘Kunshan Asia Aroma Cooperation Limited” kutoka nchini China kwa uamuzi wake wa
kuja kuekeza hapa Zanzibar.
Dk.
Shein aliyasema hayo leo Ikulu mjini Zanzibar wakati alipokuwa na mazungumzo na
ujumbe kutoka Kampuni ya “Kunshan Asia Aroma Cooperation Limited” kutoka nchini
China ambayo imedhamiria kuekeza katika kiwanda cha Makonyo, kilichopo Wawi
Pemba kwa kushirikiana na Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC).
Katika
mazungumzo hayo, Dk. Shein aliihakikishia Kampuni hiyo kuwa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar itatoa ushirikiano wake mkubwa kupitia Wizara yake ya
Biashara na Viwanda pamoja na Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC).
Dk.
Shein alitumia fursa hiyo kuipongeza Kampuni ya “Kunshan Asia Aroma Cooperation
Limited” chini ya Mwenyekiti wake Zhou Junxue kwa kusaini Makubaliano ya Awali
kati ya Kampuni hiyo na Shirika la (ZSTC).
Aidha,
Dk. Shein aliueleza ujumbe wa Kampuni hiyo kuwa Kiwanda cha Makonyo kilichopo
Wawi ni cha muda mrefu ambacho kimekuwa kikizalisha mafuta ya aina mbali mbali
hivyo, ushirikiano wa pamoja katika uzalishaji kiwandani hapo kutasaidia kuinua
ubora wa kiwanda sambamba na kuongeza pato la Taifa na soko la ajira.
Alieleza
kuwa uwamuzi wa Kampuni hiyo ni mzuri na umekuja katika wakati muwafaka ambapo
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imo katika kutekeleza Sera ya Uchumi wa
Viwanda, hivyo hatua hiyo itakuwa chachu katika kufikia malengo yaliyowekwa na
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Pamoja
na hayo, Dk. Shein alieleza kuwa Zanzibar imejaaliwa kuwa na viungo vya vyakula
vya aina nyingi ambavyo miongoni mwao vimekuwa vikitoa mafuta bora ambayo
yamekuwa ni bidhaa muhimu iliyoingia katika soko la ndani na nje ya Tanzania
yakiwemo mafuta ya makonyo, mafuta ya karafuu na mafuta ya mikaratusi.
Hivyo,
Dk. Shein aliongeza kuwa kuanza kwa uwekezaji huo kutazidi kuitangaza Zanzibar
na kuwa kiwanda cha pekee katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati
kinachozalisha bidhaa hizo za mafuta.
Sambamba
na hayo, Rais Dk. Shein alieleza haja ya Kampuni hiyo kushirikiana na ZSTC
katika kutekeleza makubaliano hayo yaliotiwa saini hapo jana ikiwa ni pamoja na
kuongeza zaidi uzalishaji huku akisisitiza suala zima la ufanyaji utafiti
katika kilimo cha mazao hayo yanazotoa mafuta.
Aidha,
Dk. Shein alisisitiza suala la mafunzo ambalo litasaidia sana kuendesha kiwanda
hicho pamoja na kuongeza uzalishaji wa bidhaa za aina mbali mbali za mafuta ya
viungo kutoka katika kiwanda hicho cha Makonyo Wawi jambo ambalo pia,
litaongeza soko la ajira hapa nchini.
Nae
Mwenyekiti wa Kampuni ya “Kunshan Asia Aroma Cooperation Limited” ya China,
Zhou Junxue alimpongeza Rais Dk. Shein kwa juhudi zake katika kuimarisha uchumi
wa Zanzibar kwa kupitia sekta ya viwanda vikiwemo viwanda vidogo na vya kati.
Mwenyekiti
wa Kampuni ya “Kunshan Asia Aroma Cooperation Limited” alimueleza Rais Dk.
Shein mikakati iliyowekwa na Kampuni yake katika kuhakikisha makubaliano
waliyosaini yanatekelezwa kwa lengo la kuleta manufaa kwa pande zote mbili.
Junxue
alimuhakikishia Rais Dk. Shein kuwa Kampuni yake itatoa mashirikiano makubwa
kwa Serikali kupitia Shirika lake la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) katika
kuhakikisha kiwanda hicho kinatoa mafuta yalio bora sambamba na kuongeza
uzalishaji wa bidhaa zitakazozalishwa katika kiwanda hicho cha Wawi.
Kampuni
ya “Kunshan Asia Aroma Cooperation Limited” ya nchini China ambayo ndio mnunuzi
mkubwa wa mafuta ya viungo vya Zanzibar tokea Julai mwaka 2017, ilitiliana
saini Makubaliano ya Awali na Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC)
katika kuendesha mradi ndani ya miaka kumi utaohusisha uimarishaji wa utendaji na
utaalamu katika kiwanda cha Makonyo Wawi.
Jambo
jengine ni uendelezaji wa mazao ya karafuu na mikaratusi ili kuongeza
uzalishaji kutoka tani 60 zinazozalishwa hivi sasa hadi kufikia tani 2,000,
ubadilishanaji
uzoefu kati ya watendaji wa taasisi hizo, upatikanaji wa mafunzo, mbinu na
upatikanaji mbegu bora za mikaratusi ni
miongoni mwa makubaliano hayo.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment