Habari za Punde

Harakati Katika Marikiti Kisiwani Pemba Wakati Huu wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

NDIZI aina ya koroboi imekuwa ni ndizi Muhimu kwa Wananchi wa Micheweni, pichani gari ya abiria ya Micheweni ikipakia ndizi hizo kutoka katika gari ya Mkoani
NDIZI mbivu aina ya Mkono mmoja ni bidhaa muhimu kwa futari katika kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, kidole kimoja kinauzwa kati ya 1000, 1500, 2000 hadi 2500, mkungu mmoja unauzwa kati ya 20000/= hadi 25000/=.
BIDHAA za Nafaka zimeonekana kuwa nyingi katika kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, huku baadhi yake bei zikionekana kuwa chini, ila njugu mawe imeweza kupanda hadi kufikia 3500/- kutoka 25000/=
MMOJA wa wachukuzi wa mizigo katika soko la Matunda na Mboga mboga Chake Chake, akiwa amebeba mikungu ya ndizi katika kiroba kwa lengo la kupeleka mnadani katika soko hilo

MMOJA ya wafanyabiashara wa nazi katika soko la Tibirinzi Chake Chake, akiwa napanga bidhaa zake ambapo fungu moja la nazi nne linauzwa 3000/=





NDIZI aina ya Mkono mmoja na mtukwe ikionekana kwa wingi katika soko la matunda na mboga mboga Chake Chake, baada ya kuteremshwa kutoka katika gari na kusubiri kupigwa mnada.(Picha na Abdi Suleiman -Pemba)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.