Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe.Hemedi Suleiman (kulia) pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Chake chake Mhe.Rashid hadid Rashid mara baada ya Swala ya Magharibi jana kabla ya Futari aliyowaandalia Wananchi na Waislamu wa Mkoa wa Kusini Pemba katika Viwanja vya Ikulu Ndogo ya Chakechake Wilaya ya Chakechake
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipojumuika na Wananchi na Waislamu wa Mkoa wa Kusini Pemba jana katika Futari aliyowaandalia Wananchi na Waislamu wa Mkoa wa Kusini Pemba katika Viwanja vya Ikulu Ndogo ya Chakechake Wilaya ya Chakechake (kushoto) Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar kabi
Baadhi ya Mashekhe wakiwa katika Futari iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein jana katika Viwanja vya Ikulu Ndogo ya Chakechake wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pembaya mbali mbali katika Mikoa ya Zanzibar ikiwa ni katika mpangilio wake wa kuwafutarisha Wananchi na Waislamu wa Wilaya mbali mbali katika Mikoa ya Zanzibar
Wananchi na Waislamu wa Mkoa wa Kusini Pemba wakiwa katika Futari iliyoandaliwa jana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein katika Viwanja vya Ikulu Ndogo ya Chakechake,Wilaya ya Chakechake ikiwa ni katika mpangilio wake wa kuwafutarisha Wananchi na Waislamu wa Wilaya na Mikoa ya Zanzibar
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein (wa pili kulia) akijumuika na Viongozi akinamama na Wananchi wengine wa Mkoa wa Kusini Pemba katika Futari iliyoandaliwa jana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,katika Viwanja vya Ikulu Ndogo ya Chakechake Wilaya ya Chakechake Pemba ikiwa ni mpangilio wake wa kuwafutarisha Wananchi na Waislamu wa Wilaya na Mikoa ya Zanzibar
Baadhi ya Akinamama wa Mkoa wa Kusini Pemba wakiwa katika Futari iliyoandaliwa jana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein katika Viwanja vya Ikulu Ndogo ya Chake chake Wilaya ya Chakechake Pemba ikiwa ni mpangilio wake wa kuwafutarisha Wananchi na Waislamu wa Wilaya na Mikoa ya Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein amefutari pamoja na wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba na kusisitiza umuhimu wa kuendeleza umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi.
Futari hiyo imeandaliwa
na Alhaj Dk. Shein kwa ajili ya wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba ilifanyika
katika Ikulu ndogo Chake Chake, ambayo ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali wa
dini, vyama vya siasa, Serikali pamoja na wananchi wa Mkoa huo.
Mke wa Rais wa
Zanzibar Mama Mwanamwema Shein nae alishiriki kikamilifu katika hafla hiyo ya
futari akiwa pamoja na viongozi wanawake wa Kitaifa na wananchi wengine wa Mkoa
huo.
Akitoa neno la
shukurani kwa niaba ya Rais Dk. Shein, Mkuu wa Mkoa huo Hemed Suleiman Abdalla aliwataka wananchi
kuendeleza amani, utulivu, umoja na mshikamano pamoja na kuendelea kuiombea dua
nchi yao ili iendelee kupata neema.
Alieleza kuwa
mafanikio makubwa yataendelea kupatikana hapa nchini iwapo mashirikiano ya
pamoja yatakuwepo na wananchi wote
wataendelea kuwa kitu kimoja.
Alieleza kuwa nafsi
zote zikiwa pamoja basi Mwenyezi Mungu ataendelelea kuleta neema na kuwasisitiza
wananchi Waislamu na wasiokuwa waisilamu kuendelea kuiombea dua nchi, viongozi
pamoja na kuwaombea wananchi wote.
Aidha, aliwataka wananchi
kuendelea kutoa mashirikiano wakati wote kwa shughuli zote za Serikali na za
kijamii kwenye maeneo yao kwa ajili ya kuendeleza umoja na mshikamano miongoni
mwao.
Sambamba na hayo, aliwataka
wananchi kuendelea kupiga vita vitendo vyote viovu kwa maslahi yao pamoja ili jina
la Zanzibar liendelee kutajika vyema.
Alitoa shukurani kwa
wananchi wote waliofika katika kufutari pamoja kwa kuungana na Rais Dk. Shein kwa
ajili ya kufanya kitendo hicho cha ibada hasa katika kipindi hichi cha mwezi
mtukufu wa Ramadhani.
Pamoja na hayo, Alhaj
Dk. Shein aliwashukuru wananchi pamoja na viongozi wote wa dini na vyama vya
siasa waliohudhuria katika futari hiyo aliyowaandalia na kupongeza jinsi walivyoonesha
upendo mkubwa kwake wa kukubali muwaliko wake huo.
Mkuu huyo wa Mkoa pia,
alimpongeza Alhaj Dk. Shein kwa kitendo chake hicho cha kufutarisha na kueleza fadhila
na ujira mkubwa anaopata mtu anaefutarisha wenziwe na thamamani ya kufutarisha.
Pia, walimuombea dua Alhaj
Dk. Shein kuendelea kuiongoza Zanzibar kwa amani na utulivu na kumuomba
Mwenyezi Mungu ili kiongozi huyo aendelee kuwafanyia mazuri kama aliyowafanyia
ambapo yote hayo yatakuwaja iwapo wote watakuwa wamoja.
Nao wananchi wa Mkoa
wa Kusini Pemba wakitoa neno la shukurani lililotolewa na Sheikh Mohammed
Suleiman kwa niaba yao walitoa shukurani kwa futari nzuri aliyowaandalia na
kuonesha furaha yao kwa kufutari pamoja kiongozi wao huyo.
Kwa niaba ya wananchi
hao, Sheikh Mohammed alieleza kuwa watu wema wanajuana kwa alama njema na Alhaj
Dk. Shein ana alama njema kwani kuna dalili zote kuwa yeye ni Mcha Mungu,
mnyeyekevu na amekuwa akimuogopa Mwenyezi Mungu pekee yake.
Sheikh Mohammed alieleza
kuwa ni neema ya kuwa na kiongozi kama huyo huku akitumia fursa hiyo kumuombea
dua ili Alhaj Dk. Shein aendelee kuwa na afya njema.
Aidha, alieleza kuwa
Alhaj Dk. Shein amekuwa karibu sana na raia wake na amekuwa haangalii wapi anapotoka
ama kabila alilonalo na badala yake amekuwa akiwasaidia wananchi wake wote bila ya kinyongo wala
ubaguzi.
Sheikh Suleiman
alimsifu Rais Dk. Shein kwa niaba ya wananchi wa Mkoa huo kwa kufanya kitendo
hicho cha kuwafutarisha katika kumi hili la mwisho la Ramadhani ambalo
linaubora na umuhimu mkubwa katika suala zima la ucha Mungu.
Leo Rais Dk. Shein
anatarajiwa kufutari pamoja na wananchi wa Jimbo la Mkanyageni huko katika
viwanja vya skuli ya Mkanyageni.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment