Habari za Punde

Rc Geita Atembelea Miradi ya Huduma za Jamii, Ahimiza Ukamilishwaji Wake kwa Wakati Mkuu wa Mkoa wa Geita

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Mandisi Robert Gabriel, akiendelea na ziara yake kutembelea miradi ya maendeleo kujionea utekelezaji wake katika kufanikisha umaliziaji wake.
 


Mhe. Mandisi Robert Gabriel ameendelea kufuatilia hatua za utekelezaji wa Miradi mbalimbali Mkoani Geita kwa kufanya ziara na kuona miradi inayotekelezwa kwa fedha za Huduma kwa Jamii (CSR) kutoka Mgodi wa Dhahabu Geita (GGM).

Ametembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa Mzunguko wa Kisasa (Round About) inayojengwa Halmashauri ya Mji wa Geita. Awapongeza mafundi, ashauri ujenzi uendelee siku zote ili kazi hiyo ikamilike kwa wakati.

Mhe. Mandisi Gabriel amesema na wasimamizi wa mradi kwa kusema, ‘zingatieni thamani ya fedha (Value for Money) na ubora, lakini pia ikibidi mnara unaojengwa ukamilike kabla ya mwaka kuisha kwa kuwa sisi waandisi tukiwa na sikikuu nchi haitajengwa’. Pia amesifu usanifu wa mchoro wa Mnara utakao kaa katikati ya Round About hiyo ukiwa na uwakilishi wa vitu mbalimbali mfano alama ya Mwenge wa Uhuru (uwakilishi wa taifa letu), Matofali ya Dhahabu (alama ya utajiri wa madini) lakini pia itakuwepo saa ambayo inaonyesha kiwango cha joto.

Kwa upande mwingine, Mhe. Mandisi Gabriel ameushukuru uongozji wa Mgodi wa GGM baada ya kutembelea na kuona jumla ya mifuko ya saruji 2,136 iliyopelekwa Halmashauri ya Mji Geita katika utekelezaji wa Ujenzi wa Miundombinu ya  Elimu na Afya kisha kujionea hatua ya uchimbaji wa msingi wa ujenzi wa Shule ya Msingi ya Kisasa inayoanza kujengwa eneo la Magogo lililotengwa kwa ajili ya Shule. Mkuu wa Mkoa kwa mara nyingine akasema; angependa kuona ujenzi wa Shule hiyo inaanza mara moja, maboma yakamilike ndani ya miezi mwili na nusu, kisha ukamilishaji ufuatie na yeye atashiriki kwa kuwa msimamizi wa shughuli ya ujenzi akizingatia thamani ya fedha hivyo aliwataka wananchi kuanza usafi mara moja kwani tayari baadhi ya vifaa vya ujenzi kwa nguvu za wananchi vipo kwenye eneo hilo.

Mkuu wa Mkoa alisisitiza kwa kusema, “kwa kuwa tunatekeleza Ilani ya Uchaguzi ya  Chama Tawala CCM, na kwa kasi ninayoiona, tukikaa vizuri kufikia mwakani, Zahanati kila Kijiji tunamaliza kabla ya Uchaguzi Mdogo wa mwaka 2019 kwani maboma yakikamilika tutakuwa juu ya asilimia 80 upande wa Sekta ya Afya. Hata kwa upande wa elimu, maendeleo siyo mabaya” aliongeza.

Alipofika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mhe.Mandisi Gabriel aliona mifuko 680 ya saruji na kupokea taarifa iliyoeleza kuwa bado mifuko 1,459 haijawasilishwa na kwamba kufikia wiki ijayo itakuwa imefika. Lakini pia aliagiza ujenzi uanze wiki inayofuata kwakuwa anapanga kutembelea utekelezaje wake.

Miongoni mwa alioambatana nao katika ziara hiyo ni pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Herman C. Kapufi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Geita pamoja na wawakilishi wa Mgodi wa Dhahabu Geita GGM


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.